Saturday 23 February 2019

DK. MENGI AJITOSA MATIBABU YA RUGE

...
Mkurugenzi Mtendaji wa ITV/Radio One, Joyce Mhavile, amesemaMwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi, yuko tayari kuchangia matibabu ya Mkurugenzi wa Vipindi vya Uzalishaji Clouds Media, Ruge Mtahaba, ambaye yuko Afrika ya Kusini kwa matibabu ya kibingwa.


Mhavile alitoa ahadi hiyo jana katika mahojiano maalum na Kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na Kituo cha Luninga ya Clouds cha jijini Dar es Salaam.



Alisema tayari amempa taarifa Dk. Reginald Mengi kuhusu kuugua kwa Ruge na ameahidi kumsaidia pindi kamati maalum iliyoundwa kukusanya michango itakapokamilisha taratibu.



“IPP media inaungana na familia na ndugu jamaa na marafiki, kumchangia fedha kwa ajili ya matibabu ya Ruge ili asimame tena. IPP ipo tayari kumchangia Ruge baada ya kumati kutoa maelekezo ya nini kifanyike," Mhavile alisema.



Alisema taarifa za kuugua kwa Ruge alizipata mwaka jana akiwa India na alipomwona, alimpa pole na anaamini Ruge atapona na kuendelea na majukumu ya kujenga taifa.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger