Tuesday 26 February 2019

ABIRIA WANUSURIKA KUFA BAADA YA TRENI KUGONGA BASI ASUBUHI HII

...

Treni ya kusafirishia abiria imeligonga basi katika mtaa wa Pipeline jijini Nairobi nchini Kenya ikitoka Embakasi.

 Ajali hiyo imetokea asubuhi ya Jumanne, Februari 26 na imelihusisha basi la kampuni ya City Hoppa na hakuna aliyejeruhiwa.

Kufikia muda wa kuchapisha ripoti hii, shughuli zilikuwa zimekwama eneo hilo huku Shirika la Reli Nchini likijitahidi kutoa huduma za kuondoa basi hilo.

Hii sio mara ya kwanza kwa ajali za aina hii kutokea na katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, kumeshihudiwa kadhaa. Mwaka wa 2018, treni iligonga lori la kusafirishia mafuta eneo la Pipeline na ajali hiyo ilisababisha msongamano mkubwa wa magari kwenye Barabara ya Outering. 

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger