Monday 21 January 2019

Rais Magufuli Ampongeza Felix Tshisekedi Kwa Kutangazwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC

...
Baada ya Mahakama Kuu ya Kikatiba ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumtangaza Kiongozi wa upinzani, Bw. Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa uchaguzi wa Urais, Rais John Magufuli amempongeza Rais huyo mteule na kumuahidi kuendeleza ushirikiano.

Rais Magufuli ametoa pongezi hizo  Januari 20, ambapo mbali na kumpongeza Rais Mteule amewapongeza pia raia wa Kongo akiwataka kuduisha  amani.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Magufuli ameandika, "Kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu ya Katiba. Ninampongeza Felix Tshisekedi juu ya uchaguzi wake kama Rais wa DRC.

"Ninapongeza pia Wakongo wote, ninawasihi kudumisha amani . Ninaahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kihistoria na wa kindugu".

Katika uchaguzi huo uliofanyika Desemba 30 2018, Mgombea Martin Fayulu alidai kuwa ndiye mshindi wa kiti hicho cha Urais, amezitaka Jumuiya za kimataifa kutomtambua Tshisekedi, akidai kuwa yeye ndiye mshindi halali wa uchaguzi huo.


from MPEKUZI http://bit.ly/2W8TI3A
via Malunde
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger