Wednesday 30 January 2019

POLISI YAMSHIKILIA MWANAUME NA MCHEPUKO KWA KUMUUA MKE WAKE

...
Mary Wambui  anadaiwa kuuawa na mume wake Joseph Kori kwa ushirikiano na mwanamke(mchepuko) Judy Wangui.

 Wangui alikuwa mfanyakazi wa zamani wa Kamangara na kulingana na ripoti zilizosambaa ni kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mume wa bosi wake.

 Inadaiwa kulitokea ugomvi uliosababisha kifo cha Kamangara na mwili wake kutupwa katika bwawa la maji Jumamosi, Januari 26.

  Dada wa marehemu Esther Kamangara alisema, dada yake alitaka kufahamu ni nani aliyetaka kuondoka na mtoto wake, Kamangara alitoka nje na kukutana ana kwa ana na Wangui aliyekuwa mfanyakazi wake wa zamani na alikuwa akishuku kuwapo uhusiano kati yake na mume wake.

  Kori alikamatwa eneo la tukio na awali alikuwa ameripoti polisi kuhusu kutoweka kwa mke wake na hata kuwapeleka polisi katika nyumba ya Wangui ambapo matone ya damu yalipatikana. 

 Joseph Kori na  Judy Wangui  wanazuiliwa kwa madai ya kuhusika na mauaji ya mke wake Mary Wambui Kamangara.

Chanzo:Tuko
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger