Thursday 31 January 2019

MBUNGE WA CHADEMA GODLESS LEMA ATANGAZA KUJIUZULU

...

Mbunge wa Arusha mjini (CHADEMA), Godbless Lema.


Mbunge wa Arusha mjini (CHADEMA), Godbless Lema amesema kuwa endapo Spika wa Bunge Job Ndugai atalithibitishia bunge kuhusu kauli yake dhidi ya matibabu ya Lissu, yeye atakuwa tayari kujiuzulu.

Lema ametoa kauli hiyo kwenye ukurasa wake wa 'twitter' ambapo amejibu kauli iliyotolewa na Spika akiwa bungeni leo ambapo amesema kuwa mpaka sasa bunge limegharamia shilingi milioni 250 katika matibabu ya mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu.

"Bunge halijawahi kumlipia Mh Lissu pesa kwa ajili ya matibabu, alichokisema Mh Spika Ndugai ni upotoshaji kwa jamii na Mungu. Chama kitatoa tamko juu ya hili. Spika akiweza kuthibitisha hili, mimi nitajiuzulu Ubunge, mshahara wa Mbunge sio hisani ya Spika", ameandika Lema.

Akizungumza bungeni leo, Januari 13 Spika Job Ndugai amesema hadi sasa Bunge limeshamlipa Tundu Lissu shilingi milioni 250 kwa ajili ya matibabu yake.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger