Tuesday 29 January 2019

KOMPANY KUTEMWA RASMI MAN CITY

...
Nahodha wa klabu ya Manchester City Vincent Kompany hatopewa kandarasi mpya kulingana na mkufunzi Pep Guardiola.

Kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 anayeichezea Ubelgiji inakamilika mwisho wa msimu huu .

Ameichezea klabu hiyo mara 14 msimu huu na sasa anauguza jeraha la misuli.


Ripoti wikendi zinasema kuwa City ilitaka kumpatia Kompany mkataba wa miezi kumi na mbili lakini hali yake ya maungo ndio ilizua wasiwasi.

Amecheza mechi tatu pekee tangu mwanzo wa mwezi Novemba huku mechi yake ya mwisho ikiwa ushindi dhidi ya Liverpool mnamo tarehe tatu Januari.

Kompany aliwasili katika klabu ya City mwaka 2008 kutoka klabu ya Hamburg na kutia saini kandarasi ya miaka sita hadi mwaka 2012.


''Sitaki klabu iseme , ni sawa unaweza kuondoka, wakati huohuo ni muhimu kujua kwamba kuna wakati ambapo ni mwisho kwa kila mtu, Ndio maana nikasema kuwa sio uamuzi wangu'', alisema Guardiola.

Chanzo:Bbc

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger