Thursday 31 January 2019

MKE AMCHOMA MMEWE KWA MAJI YA MOTO SEHEMU ZA SIRI

...
Jamaa mmoja mwenye umri wa makamo amekimbizwa hospitalini kaunti ya Kirinyaga nchini Kenya baada ya mkewe kumchoma kwa maji moto kwenye sehemu nyeti/sehemu za siri. 

Inaelezwa kuwa jamaa huyo alipigiwa simu na mmoja wa wateja wake wa kike akimjuza kuhusu nafasi ya kazi ila mkewe alidhani alikuwa akizungumza na mchepuko wake.
 
Mwanamke aliingia hadi jikoni akiwa amejawa na hasira, akachemsha maji na kisha akamumwagia mumewe kwenye sehemu zake za siri na mgongoni.

 "Nilipigiwa simu na mmoja wa wateja wangu wa kike akinieleza kuhusu nafasi ya kazi lakini mke wangu alijawa na ghadhabu na kuanza kunikashifu kwa kutokuwa mwaminifu katika ndoa," Mwathiriwa alisema. 

 "Mke wangu alienda jikoni, akachemsha maji na muda mfupi baadaye alirudi na maji moto kwenye sufuria na kunimwagilia kwenye sehemu nyeti na mgongoni," Jamaa huyo aliongezea.

 Aidha, jamaa huyo ambaye anapokea matibabu katika hospitali ya Kimbimbi alisema mkewe wa miaka 12 katika ndoa amekuwa akitishia mara kadhaa kumchoma. 

Via Tuko blog
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger