Sunday 27 January 2019

SIMBA MSHINDI WA TATU SPORTPESA..WAMEICHAPA MBAO UWANJA WA TAIFA

...
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara Simba, leo wameibuka washindi wa tatu katika mchezo wa SportPesa Cup Uwanja wa Taifa kwa kushinda mbele ya Mbao kwa penalti 5-3.

Dakika 90 za mchezo huu ambao ulikuwa na kasi kwa timu zote mashabiki walishuhudia timu zikitoka suluhu na kupelekea mwamuzi kuamua ipigwe mikwaju ya penalti.

Simba walifunga penalti zote tano huku wapigaji wakiwa ni Emanuel Okwi, Pascal Wawa, Deogratius Munish, Nicholas Gyan na Clatous Chama.

Kwa upande wa Mbao waliofunga walikuwa ni Said Khamis, Vincent Philipo na Peter Mwangosi huku Rajesh Kotecha akikosa penalti ya nne.

Kwa matokeo hayo Simba wanakuwa washindi wa tatu wa mashindano ya SportPesa Cup huku Mbao wakishika nafasi ya nne.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger