Thursday 31 January 2019

WAZIRI UMMY ATOA MABATI 200 KUSAIDIA UJENZI WA SHULE TANO ZA SEKONDARI JIJINI TANGA

...

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis Mkoba.
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa.
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis Mkoba
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee
na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Naibu Meya wa Jiji la Tanga Mohamed Haniu baada ya kumkabidhi Mkurugenzi wa Jiji hilo Daudi Mayeji
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa halfa ya kukabidhi mabati 200 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule tano Jijini Tanga kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa

***
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ametoa mabati 200 yenye thamani
ya shilingi milioni 4.2 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule tano za Sekondari Jijini Tanga. 

Halfa ya makabidhiano hayo yalifanyika mjini Tanga kwenye shule ya Msingi Mwakidila ambapo Mkurugenzi wa Jiji hilo alipokea mabati hayo ikiwa ni mkakati wa Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga kusaidia kuondosha changamoto ya uhaba wa madarasa. 

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mabati hayo, Waziri Ummy aliwashauriwa wazazi na walezi kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya watoto wao jambo ambalo linaweza kuwasaidia kufanya vizuri kwenye masomo yao. 

“Ndugu zangu wazazi na walezi hakikisheni mnafuatilia maendeleo ya watoto wenu wanapokuwa shuleni kwani nyie pia mnaweza kuchangia ufaulu wa mtoto
wako",alisema. 

Aidha pia Waziri Ummy ameahidi kuchangia
ujenzi wa madarasa kwenye shule ya Sekondari Kange ili kuchochea ukuaji wa sekta ya elimu kwa mkoa wa Tanga . 

“Lakini pia niwashukuru watendaji wa Shirika la Tawode kwa kujitoa katika kuchangia maendeleo ya Jamii ya Tanga kwa kutafuta wafadhili mbalimbali wa ndani na nje ya mkoa huu”,alisema.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger