Tuesday 29 January 2019

MAREKANI YAISHITAKI KAMPUNI YA HUAWEI KWA TUHUMA YA WIZI

...
Marekani imewasilisha kesi 23 dhidi ya kampuni ya mawasiliano ya China, Huawei.

Marekani imeishtaki kampuni kubwa ya mawasiliano ya China, Huawei na afisaa mkuu wake wa fedha, Meng Wanzhou.

Mashataka hayo ni pamoja na ubadhirifu wa fedha, kupinga utekelezaji wa haki na wizi wa teknolojia.

Kesi hiyo huenda ikazua mgogoro wa kibiashara kati ya Marekani na China hali ambayo itaathiri biashara ya kampuni hiyo.

Kampuni ya Huawei imekanusha madai hayo.

Katika taarifa, Huawei imesema kuwa imeghadhabishwa na mashtaka dhidi ya yake.

Imesema kuwa haikufanya makosa yote yanayodaiwa ilitekeleza na kwamba haina ufahamu wa kosa alilotekeleza Bi Meng.

Chanzo:Bbc
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger