Tuesday 29 January 2019

ONYO LA RAIS MAGUFULI KWA ALIOWATEUA

...
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewataka Wakuu wa Wilaya nchini kutotumia mamlaka yao vibaya kwa kuwaweka ndani baadhi ya watendaji wenzao ikiwa ni kinyume na sheria.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo Jijini Dar es salaam wakati akiwaapisha wakuu wa wilaya mbili, Mwanga pamoja na Tarime ambapo alibainisha sababu za kuwatengua waliokuwa kwenye nafasi hizo kuwa ni kutokana na kutumia vibaya mamlaka yao.

 "Mnasheria na mamlaka mlizopewa msizitumie vibaya sheria mnazo lakini msizitumie vibaya mtu anawekwa ndani halafu hamumpeleki mahakamani", alisema 
Rais Magufuli.

"Viongozi wengi wamelizungumzia hili namimi nalirudia, kuna masuala mengine hayahitaji mtu kuweka ndani yanahitaji kutoa maelekezo tu", aliongeza Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amehoji juu ya hatua mtu anayetuhumiwa kubaka watoto 11 kushindwa kukutwa na hatia na mahakama baada ya ushahidi kutojitosheleza.

Chanzo:Eatv
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger