Muuguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru Arusha Martin Chama amesimamishwa kazi ya kutoa huduma za uuguzi na ukunga kwa mwaka mmoja na Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania. Uamuzi huo ulifikiwa katika kikao cha baraza hilo cha 196 baada ya kumtia hatiani kwa makosa mawili kati ya manne yaliyowasilishwa katika baraza hilo Septemba mwaka jana na aameanza kuitumikia adhabu hiyo tangu Februari 7, 2019. Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga, Agnes Mtawa ameyataja makosa hayo kuwa ni kufika kazini akiwa amelewa na kutaka kuhatarisha usalama wa wagonjwa na ndugu zao…
0 comments:
Post a Comment