Na.Amiri kilagalila Serikali imeamua kuifumua Sheria ya Uvuvi Namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009 ili kuondoa vikwazo vya kibiashara na uwekezaji katika sekta ya uvuvi. Pia kwenda na kasi ya mabadiliko ya Serikali ya awamu ya tano inayolenga kujenga Tanzania ya viwanda, kuwatetea na kuwalinda wanyonge. Akizungumza katika uzinduzi wa ukusanyaji maoni ya wadau kuhusu rasimu ya Sheria ya Uvuvi na Sheria ya Ukuzaji viumbe kwenye maji jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina, alitaja sababu nyingine zilizosababisha kuwapo mabadiliko hayo.…
0 comments:
Post a Comment