Tuesday, 5 February 2019

MAPACHA WAZUA GUMZO BAADA YA KUOA MWANAMKE MMOJA

...
Mapacha wa kiume wamevunja rekodi nchini Afrika Kusini baada ya kufunga pingu za maisha na mwanamke mmoja.

 Ndugu hao wawili walipiga picha pamoja na mke wao huku wamevalia ngozi za chui. 

Mwanamke huyo alikuwa kati kati yao huku akiilaza mikono yake kila pande kwenye mapaja ya waume zake.

 Huku waume hao wakionyesha furaha kwa tabasamu kubwa, mwanamke huyo alionekana kama aliyechanganyikiwa.

Katika picha kadhaa zilizochapishwa katika mtandao wa Twitter na Catchvibe Moatshe, harusi hiyo iliyofanyika Jumamosi, Februari 2 iliwaacha wengi wakishangaa kuhusu jinsi ndugu hao wawili walikubaliana kumuoa mwanamke mmoja.

 Baadhi walikataa wakidai kuwa mke mmoja hawezi kukubali kuolewa na wanaume wawili.

 Walidai kuwa mume mwengine alikuwa nao kwa ajili ya picha tu wala si kwa ndoa. Suala hilo limesalia kuwa kitendawili, wengi wakijiuliza maswali bila majibu. 

Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger