Tuesday 3 June 2014

VICKY KAMATA:AFARIJIWA NA WANAWAKE WENZAKE BAADA YA NDOA KUKWAMA

...


Wabunge wanawake wenye muda mrefu bungeni pamoja na mke wa waziri mkuu, Mama Tunu Pinda juzi walimuandalia sherehe ya kumfariji mbunge wa viti maalum (CCM), Vicky Kamata baada ya harusi aliyotarajia kufunga wiki iliyopita, kukwama.
Sherehe hiyo ya faraja, ilifanyika Hoteli ya Dodoma kati ya saa 1.00 jioni na saa 6.45 usiku juzi mjini hapa.
“Unajua hata yeye mwenyewe tulim-surprise (tulimshtukiza). Alijua kuwa ni chakula cha jioni, lakini alipofika alikutana na muziki, kwaya na wabunge wengine waliompokea kwa vifijo na nderemo,” alisema mmoja wa wabunge waliohudhuria hafla hiyo. Sherehe hizo zilitumbuizwa na kwaya ya kikiristo ya Mvuke ya kanisa la Anglican mjini Dodoma.
Alisema Vicky alijua kuwa amealikwa na mbunge wa viti maalum (CCM), Magreth Sitta kwa ajili ya chakula cha jioni lakini alipofika aka kutana na sherehe.
“Tuliona ni vyema kumuandalia sherehe kidogo ili kumpa moyo kwamba hayo yametokea kwa sababu Mungu alitaka kumuepushia na mambo makubwa siku za usoni,” alidokeza mmoja wa waliohudhuria sherehe hiyo.
Baadhi ya wabunge waliohudhuria ni wabunge wa viti maalum kutoka CCM ambao ni Magreth Sitta, Anna Abdallah, Felister Bura, Hilda Ngoye, Agness Hokororo na Anastazia Wambura.
Wengine waliohudhuria ni Asumpta Mshama (Nkenge-CCM), Anne Kilango (Same Mashariki-CCM) na Waride Bakari Jadu (Kiembe Samaki-CCM). Chanzo hicho kilisema wabunge Anne Kilango, Magreth Sitta na Anna abdallah, walielezea jinsi baadhi ya wanawake viongozi walivyokumbwa na mikasa kama ya Vicky na wengine hata kuacha wakiwa makanisani.
“Wengine walieleza jinsi walivyoteswa na wenza wao na kwamba amshukuru Mungu pengine amemuepushia mambo makubwa ambayo yangeweza kutokea kama ndoa ingefungwa,”alisema shuhuda huyo.
Alisema sherehe hiyo ilikuwa kama ibada maana muda mwingi ulitumika katika kumuhubiria Vicky na kumsihi asikatishwe tamaa na badala yake asonge mbele.
Alipoulizwa kuhusu sherehe hiyo, Vicky alikiri kufanyika lakini akakataa kuielezea kwa kina.
“Mimi niliitwa kwenye chakula cha jioni lakini nilipofika pale nistaajabu kukutana na sherehe,”alisema Vicky ambaye alikataa kuelezea kwa kina kuhusu sherehe hizo.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger