Tuesday 22 January 2019

WAZIRI AGOMA KUTUMBULIWA NA RAIS MAGUFULI

...
Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema hayupo tayari kutimuliwa na Rais John Magufuli kwa kushindwa kupeleka huduma za maji kwa wananchi.

Kauli ya Aweso imetokana na kusuasua kwa utekelezaji wa miradi ya maji katika wilayani Kisarawe mkoani Pwani licha ya bajeti iliyopo.

Akizungumza leo Jumanne Januari 22, 2019 wakati wa ziara ya kikazi katika wilaya hiyo, Aweso amesema Rais Magufuli alipomteua alimpa jukumu la kuhakikisha maji safi na salama yanawafikia wananchi wote.

Kauli hiyo ya Aweso imetokana na kusuasua kwa miradi ya maji wilayani humo huku mkuu wa wilaya hiyo, Jokate Mwegelo akisema imeshindwa kuendelea kwa kukosa huduma ya maji.

"Tulipoteuliwa katika nafasi hizi Rais alisema anatupa wizara hii ili wananchi wapate maji na wasipopata basi atatumbua na mimi sipo tayari kutumbuliwa," amesema Aweso.


Na Cledo Michael, Mwananchi
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger