Wednesday 16 January 2019

SANAMU LA SHETANI LASHUTUMIWA KUFURAHI SANA

...
Sanamu la shetani linalopangwa kuwekwa katika mji wa Uhispania Segovia limeshutumiwa kwa kufurahi sana.

Sanamu hilo la shaba bronze liliundwa kwa heshima ya ngano au hadithi ya kale inayosema kuwa shetani alihadaiwa kujenga bomba mashuhuri la maji mjini humo.

Lakini wakaazi wanasema shetani huyo - anayetabasamu na anayeonekana kupiga slefie na simu ya mkononi - anaonekana kuwa na upole na urafiki mwingi.

Msanii huyo ameiambia BBC ameshangazwa na kiwango cha shutuma zilizoelekezwa kwa kazi yake.

Jaji mmoja sasa ameagiza sanamu hilo lisiwekwe kwa sasa wakati anaposhauriana kufahamu iwapo linadhalilisha Wakristo.

Chanzo:Bbc


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger