Wednesday 16 January 2019

RAIS KENYATTA : MAGAIDI WALIOUA RAIA 14 NA KUJERUHI 30, WOTE WAMEUAWA

...

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema magaidi wote waliofanya shambulio katika hoteli ya kifahari ya DusitD2 na kusababisha vifo vya watu 14, wameuawa.

Kenyatta ametoa kauli hiyo leo Jumatano Januari 16, 2019 wakati akihutubia Taifa kuhusu operesheni ya kupambana na magaidi waliovamia hoteli hiyo. Tukio hilo lililotokea jana Januari 15, 2019.

Amebainisha kuwa watu 700 wameokolewa na vyombo vya ulinzi na usalama, kwamba operesheni hiyo imekamilika na magaidi wote wameuawa.

Rais Kenyatta amesema watu 30 waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali mbalimbali za mjini Nairobi.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger