Wednesday 16 January 2019

HILI NDIO KUNDI LILILOTHIBITISHA KUFANYA SHAMBULIZI RIVERSIDE NAIROBI

...
Kundi la wapiganaji la al-shabab linakabiliana na serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa nchini Somalia na limefanya misururu ya mshambulizi katika eneo zima.
Kundi hilo linalohusishwa na al-Qaeda limefurushwa katika miji mingi lililodhibiti lakini linasalia kuwa hatari.

Neno al-Shabab linamaanisha vijana kwa lugha ya kiarabu.

Lilijitokeza kutokana na kundi lenye ititakadi kali la Muungano wa mahakama za kiislamu nchini Somali ambalo lilikuwa likidhibiti mji wa Mogadishu 2006, kabla ya kufurushwa na vikosi vya Ethiopia.

Kuna ripoti kadhaa za wapiganaji wa Jihad wa kigeni wanaoelekea Somalia kusaidia al-Shabab, kutoka mataifa jirani pamoja na Marekani na Ulaya.

Limepigwa marufuku kama kundi la kigaidi na Marekani pamoja na Uingereza na linaaminika kuwa na kati ya wapiganaji 7000 na 9000.

Al-Shabab linahubiri Uislamu wa madhahabu ya Wahhabi kutoka Saudia huku raia wengi wa Somali wakiwa wa madhahabu ya Sufi.

Limeweka sheria kali za Kiislamu katika maeneo linayodhibiti , ikiwemo kumpiga mawe hadi kufa mwanamke anayetuhumiwa kuzini mbali na kuwakata mikono wezi.

Chanzo:Bbc
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger