Sunday 20 January 2019

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 198 )

...
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  
             
“Tuondoke”        
Jojo alizungumza huku akitangulia kutoka nje, hapakuwa na msichana hata mmoja aliye jaribu kumshika wala kumsogelea Jojo. Tukapandisha juu kabisa ya meli hii.

“Ninahitaji twende nyumbani sasa baba”
Jojo baada ya kuzungumza hivyo akanikumbatia kwa nguvu kisha tukajitosa kwenye bahari na nikajikuta nikianza kupiga kelele kwani kasi tunayo kwenda nayo chini kusema kweli inatisha na kuogopesa na ukitegema ni usiku  basi ujasiri ukaniisha kabisa.

ENDELEA
Tukazama ndani ya maji cha kushangaza sipati tabu ya aina yoyote kama binadamu wa kawaida akizama chini ya maji. Tukazidi kwenda chini sana hadi kwa mbali nikaanza kuona taa nyingi zinzo waka kwa haraka haraka unaweza kuzifananisha na jiji la New York nchini Marekani pale ifikapo majira ya usiku. Nikatamani kuzungumza kitu ila nikashindwa kabisa na kusahau hata kitu hicho ninacho hitaji kukuzungumza.

Tukafika hadi kwenye moja ya jumba la kifahari ambalo kuta zake zimejengwa kwa dhahabu tupu, hakuna sehemu ya jumba hili iliyo sakafiwa hata kwa saruji.

“karibu baba hapa ndipo kwa mama anapo ishi”
Jojo alizungumza huku akiniachia. Kusema kweli kuna mambo mengi sana dunia nilikuwa ninayasikia juu ya viumbe hivi vinavyo itwa majini ila kusema kweli leo ndio nimeamini kwamba kuna mji wa majini ambao wanaishi kama tunavyo ishi duniani. Nikiwa kama binadamu wa kawaida, lazima woga unitawale hata kama nimefanya mambo mengi maovu na ya kutisha ila huku nilipo kusema kweli ninaogopa sana.

“Usiogope baba, yangu kuwa na amani”
“Ila Jojo ninaoga”
“Hakuna anaye weza kukudhuru”
Wasichana wa huku kusema kweli ni wazuri kupindukia, wana kila aina ya sifa ambayo duniani huwezi kumkuta nayo mwanamke mmoja. 

Nilihisi kwamba Magreti ana wazidi wote ila hawa wa huku wana wazidi wote waliopo duniani. Kila tunapo pita mimi na Jojo, tunamwagiwa maua na wasichana hawa ambao wamajipanga pande mbili za barabara inayo ingia kwenye jumba hili la kifahari. 

Mlango ukafunguliwa na nikakuta ukumbi mkubwa sana na mbele kabisa kuna kiti kimoja ambacha mekaa Olvia Hitler huku pembeni yake kukiwa na wasichana wawiliw alio shika manyoya makubwa ambayo sifahamu hata ni ya mnyama gani ila wanampepea taratibu.

“Waooo karibu mume wangu”
Olvia Hitler alizungumza huku kinyanyuka kwenye kiti chake, akaanza kunifwata kwa mwendo wa taratibu huku gauni lake jeupe pee likiburuzika kwa nyuma. Tukakumbatia taratibu, marashi mazuri aliyo jipulizia Olvia Hitler kusema kweli yakanisisimua mwili mzima.

“Pole sana kwa tabu za dunia ambazo umepitia”
“Asante”
“Usiogope, hapa ndipo kwangu, karibu sana, nilimuachia maagizo Jojo wako kwamba akulete pale atakapo pata nafasi ya kukuleta hapa nyumbani”
“Nimekaribia”
Olvia Hitler akapiga kofi moja, wakaja wasichana wanne walio valia vizuri na wamependeza sana.

“Mpelekeni baba Jojo mukamuogeshe”
“Sawa malikia”
Wasichana hawa wakanishika mikono yangu na taratibu tukaondoka katika ukumbi huu, tukaingia kwenyemoja ya chumba kikubwa ambacho kina swimming pool kubwa ambayo maji yake yanafuka mvuke. 

Taratibu wakaanza kunivua koti langu la suti, wakafwatia shati, na kumalizia nguo zote za chini na nikabaki kama nilivo zaliwa. Wasichana hawa nao wakavua nguo zao na kuingia nami kwenye swimming pool hili kwa mara ya kwanza nilihisi labda maji yanaweza kuwa ya moto, ila mvuke vuke wake kusema kweli yameufanya mwili wangu kuhisi nguvu fulani ambayo katika maisha yangu sikuwahi kuihisi hii nguvu.

Taratibu wakaanza kuniogesha mwili wangu, hapakuwa na sehemu ambayo wameshindwa kuigusa, hata jogoo wangu mamemgusa kwa viganja vyao vilaini ila hapakuwa na hisia yoyote kwenye mwili mwangu. 

Wasichana hawa hawazungumzi chochote na mimi, baada ya kumaliza kuniogesha wakanitoa ndani ya swimming pool hili kisha wakanivisha vazi kubwa lililo pambwa mwa madini ya dhahabu kwenye maua mau yake. Tukarudi katika ukumbi huu, na nikapokelewa na tabasamu kubwa la Jojo na mama yake.

“Baba umebadilika kama sio wewe”
“Eti ehee”
“Ndio yaani umekuwa kama mfalme fulani hivi”
“Hahaa ila ni mfalme kwa maana mimi si malikia”
“Alafu kweli mama hapo umenena jambo la kweli”

“Inabidi mule sasa alafu nikawatembeze”
“Mukanitembeze wapi?”
“Inabidi uweze kufahamu mji huu viziri sana, pia ukaione familia yako sehemu walipo”
“Familia yangu?”

Niliuliza huku nikiwa nimejawa namshangao mkubwa sana.
“Ndio familia yako”
“Twendeni sasa hivi jamani nina hamu ya kuiona familia yangu?”
“Mmmmm acha papara baba, kula alafu tutakwenda sote watatu”
Sikua na jinsi ya kufanya zaidi ya kumsikiliza Olvia Hitler anacho kizungumza. Tukaingia katika chumba cha kupatia chakula na kuanza kupata chakula taratibu. Chakula cha huku kusema kweli ni kitamu sana na kinavutia ambacho duniani sikuwa kula. Tukamaliza kula chakula na tukaanza kutembea sehemu mbali mbali za huu mji nanikajionea mambo mengi sana ambayo kusema kweli dunia hakuna kabisa.

“Huu ndio ulimwengu, ambao hakuna binadamu anaye weza kuja pasipo ridhaa yetu”
“Ni pazuri sana”
“Kwenye huu mji wetu kuna sehemu mbili, moja ni hii ambayo unaiona ni nzuri sana na kuna nyingine ambayo ni mbaya sana. Huko ndipo jehanamu, sehemu ambayo wanadamu wakifa wale ambao ni wetu basi wanaletwa huku chini”
Olvia Hitler alizungumza huku akinitazama uosni mwangu.

“Sasa familia yangu ipo wapi?”
“Familia yako ipo huko sehemu ya pili, mtu ambaye hayupo kwenye sehemu hiyo ni mmoja tu ambaye ni mwanao wa kike, ila wengine wote wapo huku”
Nikajihisi tumbo langu kunika, ila nikajikaza.

“Huku tunapo elekea unatakiwa kuwa mkakamavu sawa Dany”
“Sawa”
Nilizungumza ila moyo wote umepoteza imani. Kufumba na kufumbua tukajikuta tukiwa ndani ya sehemu yenye giza kubwa ila mianga ya makaa ya moto inatufanya tuweze kouna watu waliomo ndani ya shimo kubwa huku miili yao wakiwa hawana nguo  hata moja. Watu wote waliomo kwenye hili eneo wanaonekana kupata maumivu makali ya moto unao waunguza. Katika kukatiza macho yangu huku na kule nikamuona mama yangu akiungua jhuku  akipiga mayowe ila hakuna anaye weza kumsaidia. Nikataka kumfwata na kumsaidia, ila Olvia Hitler akanishika mkono na kunizuia.

“Unataka kwenda wapi?”
“Kumsaidia mama yangu?”
“Huwezi kwenda, hili eneo ni la muumba wa kila kitu”
“Ina maana unataka kusema kwamba humu kunalindwa na Mungu?”
“Ndio, malaika wa Mungu wanalinda hili eneo”
“Hatuwezi kweli kuwasaidia, yaani hata kufika huku, hata Jojo mwenyewe hajawahi kufika, kwa nguvu zangu ndio mume weza kufika huku. Nikamuona mdogo wangu Diana akipata mateso makali sana huku mwilini mwake akitobolewa na funza wenye moto. Nikamuona baba yangu naye akiteseka sana huku adhabu yao yote ikiwa ni moja kwa wote. Kuna baadhi ya viongozi wa Tanzania na dunia nzima nikawaona nao wakipata adhabu kubwa.

“Mama hivi hawa si waliokuwa ni viongozi?”
“Jojo huku hakina kiongozi, mtu akifa kama ana dhambi zake, breki yake ya kwanza ni hapa. Anapata kibano kama hawa, hadi siku ambayo Mungu ataamua kuimaliza dunia”
“Mmmm hivi Olvia Dunia inaweza kuisha?”
“Sio leo wala kesho kwa maana hata sisi hatufahamu ni siku gani dunia itahukumiwa”
“Mmmmmm sasa hata sisi si tutahukumia?”
“Inategemea na itakavyo kuwa kwa maana katika hilo kusema kweli hata mimi sielewi itakuwaje”
Sikuzungumza kitu chochote zaidi ya kuwatazama wana familia yangu jinsi wanavyo pata mateso makali. Huruma ikanijaa moyoni mwangu na kujikuta nikimwahikwa na machozi usoni mwangu, Jojo na mama yake wakabaki kimya. Taratibu wakanishika mkono, kufumba na kufumbua tukatoka katika hili eneo na tukatokea katika eneo jengine kabisa ambalo limetulia sana na lina nyumba moja pamoja na miti mingi.

“Huku ni duniani au?”
“Hapana bado upo chini ya bahari”
“Hivi inakuwaje hadi munaishi kama hivi?”
“Kivipi?”
“Munaishi chini ya bahari?””
“Yote ni miujiza ya Mungu”
“Hata nyinyi muna muabudu Mungu?”
“Ilikuwa, ila si kwa sasa”

“Ilikua lini?”
“Kipindi hicho kabla haijatokea vita huko mbinguni”
“Ahaaa sawa sawa”

Tukaingia ndani ya hii nyumba, alama niliyo kutana nayo kwenye tambaa kubwa lililo ning’inizwa katika hili seble.

“Dany mume wangu unatakiwa kuweza kupata nguvu ambazo zitakusaidia kwa maisha yako yote”
“Nguvu za aina gani?”
“Hapa unapo paona ndipo anapo ishia baba yangu, ambaye hadi leo bado anahistoria kubwa kwenye dunia”
“Historia gani?”
Olvia hakunijibu chochote zaidi ya kuingia katika chumba kimoja kinacho nukia manukato mazuri sana. Sikuamini macho yangu kukutana na gaidi wa mika hiyo ya 1880’s ambaye ni Adolf Hitler ambaye hadi sasa hivi duniani hakuna mtu aliyeweza kudhibitisha kifo chake. Wapo walio seme kwamba alijitosa kwenye acid(tindikali), wapo walio sema amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha baada ya kushindwa vita ya pili ya dunia. Pasipo kuambiwa chochote, nikasalimia salamu yake ya kunyoosha mkono mmoja juu, mzee huyu akarabasamu sana na taratibu akanyanyuka kwenye kitanda alicho lala na kukaa kitako. Kwa ishara ya mkono akaniita na kuninyooshea mkono wake wa kulia, nikaushika taratibu.

“Kwa miaka mingi duniani, vizazi na vizazi nilikuwa ninatafuta mtu wa kumuachia uwezo wangu, sikumuona ila wewe sasa una uwezo huo kwani umeweza kuitingisha duani kama nilivyo itingisha mimi”

Adolf Hitler alizungumza huku akiendelea kuishika mikono yangu.

“Umeifanya dunia nzima kukujua, umewafanya waandishi wengi kukuandika kwenye vitabu ambavyo vitadumu miaka kwa miaka yote duniani. Utaelezewa kwenye kila historia ya kila kizazi kwamba alikuwepo gaidi anaye itwa Dany.”
“Kuanzia leo nitakupa jina la Hitler, utaitwa Dany Hitler, hakikisha kwamba jina hili unalikuza.”
“Sawa sawa mzee”
“Watu watakuogopa mara kumi ya wanavyo kuogopa hivi sasa. Utaishi karne kwa karne hadi pale atakapo tokea mtu mwenye uwezo wa kufanya zaidi ya kile ambacho umekifanya wewe ndipo utakapo kuwa tayari kumkabidhi nguvu hizi ninazo kupatia”
Jinsi mzee Adolf Hitler anavyo zungumza ndivyo jinsi nilivyo hisi kuna vitu vikiingia mwilini mwangu.

“Hadi leo nchi yangu ya ujerumani inaitwa ‘HE’. Ni mwanaume wa nchi zote duniani, hata Marekani yenyewe pia ni She. Hakikisha kwamba Tanzania unaifanya iwe He, iwe dume kama Ujerumani sawa”
“Sawa”
“Haijalishi utaifanya wewe mwenyewe, haijalishi ataifanya raisi yoyote ajaye. Ila hakikisha kwamba nchi yako, chimbuko lako linakuwa ni nchi kubwa sana ulimwenguni”
“Nimekuelewa mzee”
Nikahisi kitu kikubwa kikiupiga mwili wangu, nikajikuta nikinyong’onyea na kuishiwa nguvu kabisa na nikapoteza fahamu kabisa.                                                                                           ***

Nikayafumbua macho yangu na kujikuta nikiwa nimelala kitandani, pembeni yangu nikamuona Jojo akiwa amekaa huku akinitazama.

“Hei baba umeamka?”
“Yaaa nipo wapi?”
“Tumerudi duniani tayari”
“Kule nimeondokaje?”
“Tumeondoka siku nyingi sana, kwa maana sasa hivi ni miezi miwili imepita tangu tutoke kule nyumbani kwetu”
“Weeee acha kunitania”
Nilizungumza huku nikikaa kitako kitandani, mazingira ya chumba ninacho kiona kwenye macho yangu sikuwahi kuyaona kabisa.

“Jojo hapa ni wapi?”
“Nyumbani kwetu, nimetafuta nyumba nzuri nina imani kwamba utaipenda baba yangu”
Nikajitazama mikono wangua ambayo kwa kumbukumbu zangu za mwisho ninakumbuka nilishikana na mzee Adolf Hitler.

“Babu yako yupo wapi?”
“Tayari amepoteza maisha, tumemuhifadhi kule kule nyumbani kwetu”
Nikashuka kitandani na kumfanya Jojo naye kusimama, tukatoka chumbani humu na  kufika sebleni, nikalitazama hili eneo taratibu. Sikuhitaji kuishie hapa nikatoka nje na kuuona ufukwe wa bahari kwa mbali huku nyumba yetu hii ikiwa imezungumkwa na maua mengi sana.

“Jojo hapa ni wapi?”
“Tupo Tanzania kwenye visiwa vya Pemba, hapa ndipo makazi yetu yatakapo kuwepo miaka yote tutakayo ishi hapa duniani”
“Ila si hatari Jojo hili eneo?”
“Sio hatari baba, hapa tulipo hakuna binadamu wa kawaida anaye weza kufika katika hili eneo kabisa”
“Kwa nini hawawezi kufika?”
“Baba hili eneo lipo mbali sana na hakuna binadamu anaye weza kufika wao wapo huko mbali sana. Hapa tutakuwa tunafanya kazi zetu zote”
“Hivi kwa jinsi ninavyo tafutwa duniani, kweli hawatoweza kuja kunikamata hapa?”
“Hapana baba jiamini, ninamini mimi mwanao. Hapa ni salama kabisa kuliko hata kule kwenye meli ya Livna sio salama kuliko hapa”

Jojo alizungumza kwa msisitizo, tukaanza kulizunguka hili eneo, huku akinionyesha baadhi ya eneo la mazoezi alilo litengeneza.

“Baba kwa sasa una nguvu nyingi, ambazo unatakiwa kuanza kufanya mazoezi kuhakikisha kwamba unaweza kuzi contro nguvu zako na zisiweze kumdhuru mtu asiye na hatia”
“Mbona sihisi chochote”
“Ngoja?”
Jojo akanisukuma kwa haraka sana na nikajikuta nikianguka, hata kabla sijafika chini nikajihimili na kusimama haraka sana jambo ambalo si rahisi kwa hata mfanya mazoezi kufanya hivi”
“Baba una nguvu ya kuona kile ninacho kiona mimi, mambo yanayo weza kutokea miaka kwa miaka, pia unaweza kukwepa kitu chochoye kinacho kufwata kwa kasi ambayo binadamu wa kawaida hawezi kukiona.”
“Kama kitu gani?”
“Risasi ni moja wapo ya kitu ambacho unaweza kukikwepa haraka iwezekanavyo. Baba sasa huu ndio wakati wa kwenda kumtoa K2 madarakani, tummalize yeye pamoja na maadui wengine wote ambao waliweza kukuletea tabu wewe sawa”
Maneno ya Jojo yakanifanya nitabasamu kwani kwa uwezo nilio nao sasa K2 na wajinga wezake watajuta kunifahamu na watajutia ni kwa nini waliweza kuniharibia maisha ikiwemo kuwaua ndugu zao ambao nimewashuhudia wakipata mateso makubwa kuzimu, mateso ambayo K2 na wezake nao pia wanastahili kuyapata kwani ni haki yao.

  ITAENDELEA
‘Haya sasa Dany amepata uwezo mkubwa wa kufanya chochote juu ya maadui zake je kazi yale hiyo ataitendaje? Usikose sehemu inayo fwata ya hadi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”


from MPEKUZI http://bit.ly/2QYhETf
via Malunde
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger