Wednesday 25 May 2022

JAMES MBATIA ASIMAMISHWA KUJIHUSISHA NA SIASA ZA NCCR - MAGEUZI

...

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini imebariki uamuzi wa Halmashauri Kuu ya NCCR - Mageuzi ya kumsimamisha Mwenyekiti wa Chama hicho pamoja na Sekretarieti yake yote.

Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza amesema ofisi hiyo ya msajili inamsimamisha mwanasiasa huyo kujihusisha na siasa za chama hicho hadi pale uamuzi mwingine ndani ya Chama hicho utakapotolewa.

Ameeleza kuwa uamuzi wa Halmashauri kuu ya chama hicho ulikuwa halali kwa kuwa akidi ya kikao husika ilikuwa imetimia.

Mwishoni mwa wiki iliyopita siku ya Jumamosi Mei 21 mwaka huu, Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi ilimsimamisha Mbatia na makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi mkutano mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma zinazowakabili.

Chanzo - EATV
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger