Stori: Francis Godwin, Risasi Jumamosi
DODOMA: Katika hali
isiyo ya kawaida bibi kikongwe mmoja ambaye hakuweza kujulikana jina
lake, amezua sintofahamu baada ya kukutwa nyumbani kwa Waziri wa Kilimo,
Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba akizunguka nyumba yake usiku huku
akiwa na tunguri na wembe wenye damu.
Akizungumza na mwandishi wetu, eneo la
tukio, shuhuda wa tukio hilo, Sumai Juma alisema kuwa alimwona mwanamke
huyo akiwa amekumbatia vitu vyake akizunguka nyumba ya waziri.
Hata hivyo, alisema baada ya kumkamata
walichunguza mzigo aliokuwa amebeba ambao ulifungwa katika kanga,
kulikuwa na kuni kama 17 hivi, kikopo chenye vitu kama ungaunga mweusi
mfano wa vumbi, mkaa na wembe aina ya Topaz uliokuwa haujafunguliwa ila
ulikuwa umelowa damu.
Hata hivyo, alitoa wito kwa Watanzania
kuendelea kuliombea taifa kwani kazi kubwa ambayo serikali ya Rais Dk.
John Pombe Magufuli inayofanya ni tunu kubwa ya nchi yetu.
0 comments:
Post a Comment