Friday 19 July 2019

Ukweli Kuhusu Samaki Mtu Wa Baharini.

...
IMESIMULIWA  NA DOKTA.  MUNGWA  KABILI,   SIMU  0744 -  000  473.

Nimeulizwa  kuhusu  swali  hili  mara  nyingi sana. Watu  wengi sasa wanataka  kusikia  kutoka  kwangu  kuhusu  viumbe  hawa  wa  kipekee.

Kwa  sababu  siwezi  kumjibu  mtu mmoja  mmoja  leo  nimeamua  kutoa  majibu  ya  ujumla  kwa  watu  wote.

SAMAKI   MTU   NI  NINI?
Samaki    mtu  ni jinni  wa  baharini  ambae  hujidhihirisha  katika ulimwengu  wa  nyama  kupitia  ‘ masafa’  ya  umbo  la  mchanganyiko  wa  samaki  na  mwanadamu.

 Kuna  sababu  kubwa  sana  na  ya  msingi  kwa  nini  jinni  huyu  hujidhihirisha katika  umbo  la  samaki  na  mtu.

Labda  tu  kwa  wale  wasio  fahamu, majini  wanapo  amua  kujidhihirisha  katika  ulimwengu  wa  nyama na damu  huwa  wanafanya  hivyo  kwa  kutumia  ‘masafa’  ya  wanyama  mbalimbali  kama vile   nyoka, paka, nge nakadhalika. Ndio  maana  nyoka  wengi  wana  tabia  za  kupotea  potea  kila  wanapo  onekana.  Mnaweza  kuwa  mmekaa nyumbani  akatokea  nyoka  mkaanza  sekeseke  la  kumpiga, mara  kaingia  uvunguni  mara  ghafla  haonekani, mkiona  hivyo  basi  kuna  uwezekano  mkubwa  sana  nyoka  huyo  alikuwa  jinni.  Haya  sasa  tuendelee  na  samaki  mtu.

SAMAKI  MTU  WANAPATIKANA  WAPI ?
Samaki mtu  wanapatikana  baharini.

UMESEMA SAMAKI   MTU   WANAPATIKANA   BAHARINI  LAKINI  MBONA  KILA MARA  HUWA  TUNAENDA  KUOGELEA  BAHARINI  NA  HATUJAWAHI  KUONA  SAMAKI  MTU  HATA  SIKU  MOJA ?

Huwezi  kuwaona  samaki  mtu  ufukweni.   Ndani ya  bahari Samaki  mtu  hupatikana  kwenye  maeneo  yenye  vina  virefu. Hata siku  moja  huwezi  kumuona  samaki  mtu maeneo  ya  ufukweni.  Majini  wote  wa  baharini  wenye  nguvu  za  juu au  wale  walio  katika  daraja  la  juu, huwa  wanapatikana  kwenye  sehemu  zenye  vina  virefu.

 Kamwe  huwezi  kuwaona  ufukweni.   Hata  hivyo, majini  walio  katika  koo  nyinginezo za  majini  wanaweza  kuonekana  ufukweni  kwa  sababu  maalumu  sana  lakini  sio  Samaki mtu.

Samaki  mtu  hawezi  kuonekana  ufukweni  hata  itokee  nini!!!   Na  akitokea  ufukweni  labda  uwe  ni  ufukwe ulio  kwenye  kisiwa  kilichopo  kati  kati  ya  bahari kwenye  kina  kirefu na  pili  katika  kisiwa  hicho  kusiwe  na  shughuli  yoyote  inayo  muhusisha  mwanadamu.  Ipo sababu  ya  msingi  sana  ambayo  ina mfanya  samaki  mtu  asionekane  ufukweni hasa  hasa  katika  ufukwe  ambao  una tawaliwa  na  pilika  pilika  za  mwanadamu.

UMESEMA   SAMAKI   MTU  HAWEZI  KUONEKANA  WALA  KUTOKEA KWENYE  UFUKWE  WENYE  SHUGHULI  NA  PILIKA  PILIKA  ZA  BINADAMU.  SABABU   NI   NINI ?

Kuna  sababu  kuu  mbili  katika  hili, lakini  kabla  sijaanza  kuelezea  sababu  hizo  ngoja  nikukumbushe  kitu kimoja  muhimu  sana.  Baharini  wanaishi  majini  waswafi  tu. Baharini  hakai  jinni mchafu  wa kisheitwani. Baharini  hakikai  kitu  chochote  kichafu.  Ndio  maana  mtu  akifariki   baharini  basi  mwili  wake  unatupwa  nchi  kavu. 

Uchafu  ninao  uzungumzia  hapa  ni  uchafu  wa  kiroho yani  kitu  chenye  nguvu  hasi.   Hata  ndugu  zangu  wavuvi  wakiwa  kwenye  shughuli  zao  baharini  wanajua  kwamba  hawatakiwi  kuingia  kwenye  shughuli  wakiwa  wachafu  ( Mfano  wakiwa  na  Janaba  nakadhalika ).  Sio  hivyo  tu, bali  hata  lugha  wanayo  takiwa  kutumia  wakiwa  baharini  inatakiwa  kuwa  lugha  swafi  na  yenye  staha. Hakuna  lugha  za  matusi  wala  maneno  ya  hovyo  baharini.  Walio diriki  kuzunguma  maneno  ya  hovyo  wakiwa baharini  walipata  habari  yao.

Baharini kila  kitu  ni  kisafi.  Hata  kwa  wewe  menye  nuksi, balaa  na  mikosi  ukienda  kuoga  maji  ya  baharini  utaondosha  nukushi  zako  zote, kwa  sababu  hakuna  nguvu  hasi  inayo  weza  kukatiza  baharini.

Sasa  basi  kama  nilivyo  sema  hapo  juu  kwamba  baharini  hakikai  kitu  kichafu.  Samaki  Mtu  ni  jinni  wa  baharini. Ni  jinni  mswafi. Hakai na  kitu kichafu.  Sio  tu  kwamba  ni  jinni  wa  baharini  bali  pia  ni  jinni  anae  pendwa  na  majini  wa  baharini  kuliko  jinni  mwingine  yoyote  yule.

Kila  jinni  wa  baharini  anampenda  jinni  huyu.  Ni  jinni  mwenye  kuwavutia  sana  majini  wa  baharini. Popote  anapokuwa  anatembea  jinni  huyu  huwa  anafuatwa  na  jinni kutoka  katika  kila  koo  ya  majini  wanao  patikana  baharini.

Kwa  hiyo  popote  anapokuwa  jinni  huyu  huwa  ana  ambatana  na  majini wa  aina  zote  wa  baharini.  Ni  mfano wa  ndege  wa  porini   aitwae Msese  (Yule  mwenye  mkia  mrefu)   ambae  kila  mahali  anapokwenda  hufuatwa  na  kundi  la  ndege  lakini , Samaki  Mtu ni  zaidi  ya  Msese  kwa  sababu  Msese  hufuatwa  na  ndege  lakini  sio  ndege  wote.

Ni  kama  ndege  mmoja  wa  porini  anae  patikana  kwa  wingi  huko  kusini  mwa  Tanzania. Ndege  huyo  anapo taka  kujenga  kiota  chake, kila  ndege  unae  mjua  wewe  hupeleka  jani  kwa  ajili  ya  kujenga  kiota  cha ndege  huyu  mwenye  maajabu. Ninaposema  ndege  wote namaanisha  ndege  wote,  kuanzia  ndege  warukao  mchana  hadi  wale  warukao  usiku.

Kwa  wanyama  wanao  patikana  nchi  kavu, jinni  huyu  naweza  kumfananisha kidogo na  mnyama  aitwae Ngekewa( Mnyama  wa  porini  anaependwa  na  kuhusudiwa  na  wanyama  wote )

SABABU KWA NINI  SAMAKI  MTU  HAWEZI  KUONEKANA  UFUKWENI, HASAHASA  KWENYE  UFUKWE  WENYE  SHUGHULI  NYINGI  ZA  MWANADAMU.

Katika  ulimwengu  wa  kiroho, samaki  mtu  ni  kiumbe mwenye  uhusiano  mkubwa  sana  na  mwanadamu. Na  ndio maana  anapo  jidhihirisha  katika  ulimwengu  wa  nyama  hujidhihirisha  katika  umbile  la  mwanadamu  na  samaki. Kuna  maana  na  sababu  kubwa  sana katika  hili.

Katika  uliwmengu  wa  kiroho   lipo  jambo  moja  la  rohoni  ambalo  samaki  mtu  anafanana  sana  na  binadamu.  Nalo  ni  asili  ya   NAFSI  zao.    Asili  ya  nafsi  ya  mwanadamu  ni  UMEME-SUMAKU.  Yani  ni  umeme  wenye  sumaku  yenye  uwezo  wa  kuvuta  na  kukusanya  vitu  mbalimbali.   Ndio  maana  kijana mwenye  tabia  nzuri  anapo  anzisha  urafiki  na  kundi  la  vijana  wenye  tabia  mbaya  baada ya  muda  Fulani  na  yeye  ataanza  kuwa  na  tabia  mbaya  kwa  sababu  nafsi  yake  itakamatana  na  nafsi  za  vijana  hao  wenye  tabia  zisizo  faa (  Ndio  maana  mzazi  unashauriwa  kuchunga  sana  aina  ya  marafiki  wanao  ongozana  na  mtoto  wako  )

Hii ni kwa  sababu  nafsi  za  mwanadamu  zina  tabia  ya  KUKAMATANA  NA  KUSHIKAMANA. Na  ndio  sababu  wapenzi  wakiachana  nafsi  zao  huwa  zinapata  tabu  sana.  Humuwia  vigumu  sana  mtu  kuishi  bila  mpenzi  wake  ambae  wamezoeana na  nafsi  zao  zimekatana.

Vivyo  hivyo  na   kwa samaki  mtu. Asili  ya  nafsi  ya  samaki  mtu  ni  UMEME-SUMAKU. Nafsi  hii  inaweza  kukamatana  na  nafsi  ya  mwanadamu.

Samaki  mtu  anapokuwa  katika  mazingira  yenye  watu, nafsi  yake  huvuta  na kukamata  MAWAZO na  FIKRA  za  watu  wote  waliopo  katika  eneo  hilo  kwa  wakati  huo  jambo  ambalo  humletea  shida  sana kwa   sababu  nafasi  ya  mwanadamu  inatawaliwa  na  mambo  ambayo  hayatakiwi  kukaa kwenye  nafsi  ya  samaki  mtu.

Nafsi  ya  mwanadamu  inatawaliwa  na  mambo  makuu  yafuatayo:

1.     MAWAZO  MACHAFU  : Asilimia  kubwa  ya  mambo  anayo  yawaza  mwanadamu  ni MAWAZO  MAOVU.  Uzinzi, uasherati, husda, kijicho, usengenyaji, wivu  nakadhalika.  Haya  ni  mawazo  machafu  ambayo  hayatakiwi  kukaa  ndani  ya  nafsi  ya  Samaki  mtu  wala  nafsi  ya  kiumbe  yoyote  wa  kiroho  aishie  baharini.

Na  sababu  nimesha  ielezea  hapo  juu. Baharini hakikai  kitu  kichafu. Nafsi ya  samaki  mtu  haikai  na kitu  kichafu.   Kwa  kuwa  Samaki  Mtu  hapendi  na  hawezi  kukaa  na  vitu  vichafu. Vitu  vinavyo weza  kunajisi  nafsi  yake, kiumbe  huyu  hukaa  mbali  kabisa  na  mahali  wanapo  kaa  wanadamu  kwa  sababu  ya  kulinda  usafi  wa  nafsi  yake.

Samaki  mtu  hujisikia  vibaya  sana  kuona viumbe  wanao  fanana  na  wao  ( Yani  sisi binadamu )  na  ambao  wapo  katika  daraja  la  juu  sana  la  kiroho  miongoni mwa  viumbe  wanaoishi  duniani ( Binadamu  ndio  kiumbe  wa  Mwenyezi  Mungu  alie  katika daraja  la  juu  kabisa  la kiroho  miongoni  mwa  viumbe  wote  walioumbwa nae )  akiwa  amebeba  mambo  machafu yasiyo endana  na  hadhi  yake  ya  kiroho.

Mfano  wake  ni  sawa  tu  na  wewe  mwanaume  rijali  ambavyo  huwezi  kukaa  sehemu moja  na  wanaume  mashoga  na  kusikiliza  mambo  wanayo  yaongea. Watazungumza  mambo  yatakayo  ichefua  sana nafsi  yako. Utahuzunika  sana  kuona  wanaume  kamili kama  wewe  wakiwa  wanawaza  mambo  yaliyo  kinyume.   Na  kitu  kikubwa  utakacho  weza  kukifanya     ni  kuondoka  katika  eneo  hilo.  Hutotaka  kabisa  kukaa  karibu  na  watu  hao.   Ndivyo  ilivyo kwa  samaki mtu.

2.     MAWAZO   YA  MAHANGAIKO  NA  HUZUNI  YA  MWANADAMU Nafsi ya  mwanadamu  pia  imetawaliwa  na  huzuni  nyingi. Magonjwa  yasiyo  pona, maradhi ya  kichawi, ugumu  wa  kupata  rizki, matatizo  katika  ndoa , hofu, mashaka nakadhalika   ni  mambo yaliyo  tawala  nafsi  za  wanadamu.  Samaki  mtu  anapokaa  katika  eneo  lenye  watu  wengi  huweza  kuvuta  na  kukamata  mawazo  haya  ya  huzuni  yaliyo  tawala  nafsi  za  wanadamu.

Mawazo  haya  kwanza  humtia  huzuni  sana  kiumbe  huyu  kuona  viumbe  wanao  fanana  na  yeye  wakiwa  katika  mahangaiko  na  mateso  makubwa.  Huzuni, hofu, mashaka  na  kadhalika  ni  mambo  ambayo  hayatakiwi  kukaa  kwenye  nafsi ya  Samaki  Mtu  kwa sababu  kiumbe  huyu  ameumbwa  kuwa  na  furaha  wakati  wote. Huzuni  hizo  za  wanadamu  huchefua  nafsi  yake na  kuisononesha.  Kuepukana na  kadhia  hiyo, kiumbe  huyu  hapendi  kabisa  kukaa  karibu  na  wanadamu.

Mfano  wa  huzuni  na  sononeko  analo  lipata  hapa  ni  hapa  ni  ule  ambao  unaupata  wewe  mwanadamu  ( mwenye  moyo swafi )  ukimuona  binadamu  mwenzako  akiwa  kwenye  matatizo  makubwa. Mfano imetokea  ajali watu  wamepondwa  pondwa na  gari wamekufa  vibaya.  Kuna  watu  yakitokea  matukio  kama  haya  huwa  hawataki  hata  kuangalia na  kama  ni  kwenye  TV huwa  wanazima kabisa.

Mfano  mwingine  ni  kuona  maiti  za  binaadamu  wenzako. Watu  wengi  wana  hofu  ya  kutazama  miili  ya  marehemu  na  ni  wachache  wanaweza  kusogea  na  kukaa  sehemu  ambazo  kuna  miili  ya  watu  walio  kufa.

Kuona  maiti  ya  mtu  unaempenda  sana. Watu  wengi  hushikwa  na  huzuni  sana  pindi  wanapo  ona  maiti  za  watu  wao  wa  karibu. Huhuzunika  sana  hutamani  wasione  kabisa.    Ndivyo  ilivyo  kwa  samaki  mtu. Ndio  maana  hawapendi kukaa  karibu  na  mahali  walipo  binadamu.

UMESEMA  SAMAKI  MTU  WANAPATIKANA  KWENYE  VINA  VIREFU  BAHARINI  LAKINI  MBONA  HUWA  TUNAPITA  KWENYE  MAENEO  HAYO  LAKINI  HATUWAONI?

Huwezi  kumuona  Samaki  Mtu  kwa  sababu yupo  katika  ‘masafa’ tofauti  na  masafa  uliyopo  wewe.  Hwezi  kumuona  kwa  macho  ya  nyama  na  damu.

Viumbe  tuliopo  duniani  tunaishi  katika  masafa  tofauti  tofauti.  Ndio  maana  viumbe  wengine  mfano  majini hawaonekani  kwa  sababu  wapo kwenye  masafa  tofauti  na  binadamu  ingawa  tunaishi  nao  katika  dunia  hii  hii.

Mfano  wake  ni  sawa  na  redio  yako .  Ukiwa  na  redio  yako ukiweka  mfano masafa  namba  moja  unapata  matangazo  ya  redio  Fulani, ukiweka  masafa  namba  mbili  unapata  matangazo  ya  redio  nyingine  nakadhalika  nakadhalika.

Ndivyo  ilivyo  kwa  binadamu  na  majini. Tunaishi  nao majumbani  mitaani, tunapishana  nao barabarani, njia  panda, vyooni, makaburini  nakadhalika  lakini  huwezi  kuwaona  kwa  macho  ya  damu  kwa  sababu  wao  wapo  kwenye  masafa  ya  juu  kuliko  masafa yako  mwanadamu.

Vivyo  hivyo  kwa  samaki  mtu.  Huwezi  kumuona  kwa   macho  ya  damu  na  nyama  kwa  sababu  yeye  ni jinni  na  yupo  Kwenye  masafa  tofauti na  masafa  ulyopo  wewe.

JE  NIKITAKA  KUMUONA  SAMAKI  MTU  NINATAKIWA  KUFANYA  NINI ?

Ukitaka  kumuona  samaki  mtu  kwanza  unatakiwa kuwa  katika  masafa  yake . Yani  kuwa  na  uwezo  wa  kuona  vitu  visivyo weza  kuonekana  kwa  macho ya  nyama  na  damu.  Unaweza  kupata  uwezo  huo  kwa  kufanya  mambo  yafuatayo :  Kwanza  hakikisha  una  moyo  mswafi. Yani  ndani  ya  nafsi  yako  usiwe  na  wazo  lolote  hasi. Uzinzi, uasherati,. Husda, kisasi, kinyongo  nakadhalika.  Pili  usiwe  na  uchungu  wala  huzuni  ya  kiwango  chochote  ndani  ya  nafsi  yako.  Uwe  na  moyo  wenye  furaha  wakati  wote. Tatu  usiwe  na  tamaa  ya  kupata  chochote . Yani  lengo  lako  liwe  tu  unataka  kumuona tu jinsi  alivyo  na  sio  unataka  kumuona  kwa  ajli  ya  kupata  faida  yoyote  kutoka  kwake.

Baada  ya  hapo  uende  kwenye  kisiwa  kilichopo  baharini . Kisiwa  kiwe  kwenye  kina  kirefu  na  kusiwe  na  shughuli  zozote  za  binadamu katika  eneo  hilo.  Baada ya  kufika  kwenye  kisiwa  hicho, utafunga  na  kufanya  dua  ya  kuomba  kumuona  kiumbe  huyu. Ikiwa  ni  bahati  yako   kiumbe  huyu  atakutokea  na  utamuona. Na  asipo  kutokea  laivu  basi  anaweza  kukutokea  katika ndoto.

Kama  unaona  itakuwa  vigumu  kwenda  kwenye  kisiwani  unaweza  kufanya  ombi  maalumu  la  kumuona  Samaki  huyo katika  ndoto.  Utatakiwa  kutimiza  vigezo  vyote  nilivyo  vitaja  hapo  juu  yani  uwe  na  moyo  mswafi, usiwe  na  huzuni ( uwe  na  furaha wakati  wote ) na  usisukumwe  na  tamaa  ya  kupata  kitu  chochote  kutoka  kwa  samaki  huyo.

Kila siku  utakuwa  unaenda  ufukweni. Utakuwa  unaingia  kuogelea  kama  waingiavyo  watu  wengine  na  ukiwa  ndani ya  maji  uwe  una fanya  maombi  yako  yani  uwe  unaomba  kuonyeshwa  Samaki  Mtu  kupitia  ndoto.

Ufanye  hivyo  bila  kuchoka  wala  bila  kuwa  na  haraka  ya  kupokea  majibu  yako.   Baada  ya  muda  Samaki  huyu  atakutokea  katika  ndoto. Utamuona  Katika  ndoto.   Kama  ni  bahati  yako  basi  atakutokea  katika  ndoto  baada  ya  muda  mfupi  lakin,  Inaweza  kukuchukua  siku  arobaini, inaweza  kuchukua  miezi  mitatu, miezi  sita, mwaka  mzima, miaka  mitatu hata  Zaidi  ya  hapo.  Utakacho  takwa  kufanya  ni  kuwa  mvumilivu.  Na  kadri  utakavyo  kuwa  mvumilivu  ndivyo  utakavyo  kuwa  katika  nafasi  nzuri  ya  kumuona  samaki  huyo.

·       Je  Samaki  Mtu  wanaongea ?
·       Kama  wanaongea  huwa  wanaongea  lugha  gani ?
·       Ni kweli  samaki  mtu  huwa  wanasuka  nywele  zao ?
·       Ni kweli  samaki  mtu  huwa  wana  wabembeleza  na  kuwanyonyesha  watoto  wao ?
·       Je  kuna  uhusiano  wowote  ule  wa  vinasaba  vya  kiroho kati  ya  Samaki  Mtu  na  Mwanadamu ?

·       Kuna  dawa  moja  ya  asili  inajulikana  kama  AMBARI  NYEUPE  YA  BAHARINI.  Dawa  hii  inatumika kufungua  vifungo  vya  aina  zote na  kuwafukuza  majini  wabaya  mwilini,kwenye  biashara  na  kwenye  miji . Lakini  pia  dawa  hii  inatumika  katika  tiba  ya  kurefusha  na  kunenepesha  maumbile  ya  kiume. Kuna  watu  wanasema  dwa  hii  inatokana  na  nyangumi  na  wengine  wanasema  dawa  hii  inatokana  na  Samaki  Mtu.  Je  Ukweli  ni  upi ?

Yote  haya  nimeyaelezea  kwa  undani sana kwenye  kitabu  changu kiitwacho  " MESENJA  WA  BAHARINI "  ambacho  kitakuwa  mitaani  kuanzia  tarehe  01  SEPTEMBA 2019.  

Kitabu  kitapatikana  nchi nzima  kwenye  maduka  ya  kuuza  vitabu  pamoja  na  kwenye  vibanda  vya  wauza  magazeti.  Nchi jirani  kitabu  hiki  kitapatikana  pia  Mombasa, Nairobi na  Lamu  nchini Kenya.

Mbali  na  kuelezea  kwa  kina  kuhusu  Samaki  Mtu,ndani  ya  kitabu  hiki utapata  kujua  kuhusu  vitimbi  mbalimbali vinavyo watokea  binadamu  wakiwa  baharini  pamoja  na  mambo  yote  muhimu  yanayo  husiana  na  ufalme  wa  baharini.

IMESIMULIWA  NADOKTA.  MUNGWA  KABILI.  ANAPATIKANA  KUPITIA  SIMU  NAMBA  0744 -  000  473.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger