Monday 29 July 2019

Mbowe azuiwa kufanya mikutano Kumpisha DC Sabaya

...
Jeshi la Polisi Wilaya wa Hai limemtaka Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe kusitisha mikutano aliyopanga kuifanya kwa sababu DC Lengai Ole Sabaya anafanya ziara, hivyo mikutano itaingiliana, jambo linaloweza kusababisha uvunjifu wa amani.

 Ziara hiyo ya Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema ilitakiwa ianze leo lakini iliahirishwa jana Jumapili Julia 28, 2019 baada ya mbunge huyo kufiwa na kaka yake, Meja Jenerali Alfredy Mbowe.

Leo Jumatatu Julai 29, 2019 barua iliyotolewa na Mkuu wa Polisi wilayani ya Hai, Lwelwe  Mpina yenye kumbukumbu namba MB/JH/27/07/2019  kwenda kwa katibu wa mbunge (Mbowe) imezungumzia kusitishwa kwa ziara hizo za Mbowe.

Zuio hilo litakoma DC akimaliza ziara yake; “Kwa busara, sitisha ziara na mikutano unayotegemea kuifanya  hadi mkuu wa wilaya atakapomaliza ziara yake,” inasomeka barua hiyo


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger