Wednesday 31 July 2019

MKUU WA MKOA WA MARA AZINDUA KAMPENI YA 'NYUMBA NI CHOO'

...
Mkuu wa mkoa wa Mara Adam Malima

Na Asha Shaban - Mara
Zaidi ya kaya 22,540 zinadaiwa kuwa na ukosfu wa vyoo bora katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara jambo ambalo linafanya kaya hizo kujisaidia sehemu zisizo rasmi ikiwemo ndani ya Ziwa Victoria.

Kufuatia kuwepo kwa idadi kubwa za kaya kukosa vyoo mkuu wa mkoa wa mara Adam Malima alitoa agizo la muda wa siku 60 kwa wakazi wote wa mkoa huo ambao hawana vyoo kujenga vyoo hivyo ili kuepuka maambukizi ya magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.

Akizindua kampeni ijulikanayo kama nyumba ni choo kampeni inayolenga kuhamasisha matumizi ya vyoo katika jamii mjini hapa jana Mkuu wa mkoa alisema kuwa ni aibu kubwa kwa wakazi wa mkoa huo kushindwa kujenga vyoo na kuvitumia ipasavyo katika zama hizi na kwamba atakayeshindwa kutekeleza agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

Mbali na kutoa muda huo lakini pia Mkuu huyo wa mkoa aliwaagiza wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo kutoa taarifa ya upatikanaji na matumizi ya vyoo bora kila baada ya miezi mitatu lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa vyoo bora vinakuwepo kutumika ipasavyo muda wote.

Malima aliwataka wakazi wa mkoa wa Mara kuachana na mila potofu ambazo ni miongoni mwa sababu zinazochangia matumizi hafifu ya vyoo huku akifafanua kuwa zipo baadhi ya jamii ambazo baba anashindwa kutumia choo kimoja na watoto pamoja na wanafamilia wengine hivyo kusababisha kaya kukosa choo

Awali Afisa afya wa mkoa wa Mara, Dk. Bumija Mhando alisema kuwa hadi Desemba 2018 ni asilimia 55 tu ya kaya za mkoani Mara ndiyo zenye vyoo bora huku asilimia 38 zikiwa na vyoo vya asili na asilimia saba zikiwa hazina vyoo kabisa.

Dk. Mhando Aliongeza kuwa takwimu pia zinaonyesha ni asilimia 6 tu ya wakazi wa Mara ndio wananawa mikono kwa maji safi na sabuni baada ya kutoka chooni jambo ambalo linahitaji jitahada zaidi kuhamasisha na kuelimsiha jamii juu ya umuhimu wa kunawa mikono mara baada ya kutoka chooni.

Naye Mkuu wa wilaya ya Musoma, Dk. Vicent Naano alisema kuwa anakusudia kuwachukukia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kutoza faini kuanzia sh 20,000 kwa mkazi yeyote wa wilaya yake ambaye atashindwa kujenga na kutumia choo ipasavyo.

Alisema kuwa kufuatia kampeni iliyoendeshwa na serikali wilayani Musoma wakazi wengi wa wilaya hiyo waliweza kujenga vyoo huku changamoto kubwa ikiwa ni matumizi sahihi ya vyoo hivyo kwavile wapo baadhi yao wanajisaidia porini na ziwani.

"Sasa hivi tutaanza msako wa nyumba kwa nyumba kuangalia kama vyoo hivyo vinatumika kwavile tumegundua kuna vyoo vimejengwa kwaajili ya ukaguzi huku mkisema ni choo cha DC sasa nakuja kuangalia kama kweli hicho choo kinatumika au ni cha DC", alisema Naano.

Nyakwesi Majura ni mwananchi wa manispaa ya Musoma alisema katika mila yao hawawezi kushea choo moja na baba mkwe wake hivyo hata kama choo kupo basi kinakuwa hakitumiki kwa kuofia kuvunja miiko iliyopo ndani ya mila zao.

Alisema kuwa kwa sasa wanaanza kubadili tabia kutokana na elimu wanazo zipata na kujua madhara ya kujisaidia hovyo kuwa yanaleta magonjwa ya mlipuko na kuwa ni uchafuzi wa mazingira. 

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger