Wednesday 31 July 2019

Waziri Kigwangalla atoa siku Saba kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania

...
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Khamis Kigwangalla, ameipa siku saba Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), kuhakikisha wanapeleka mapendekezo ya namna gani watawahakikishia wawekezaji malighafi.

Katika mapendekezo hayo, amewataka kila mwaka walau kwa kipindi kisichopungua miaka mitano waweze kukopesheka kwa urahisi.

Dk. Kigwangalla amesema hayo, alipokuwa akizungumza katika mkutano wake na wadau wa Sekta ya Misitu uliofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambapo amesikiliza changamoto zinazowakabili na kuahidi kuzifanyia kazi.

“Kuhusu suala la mikataba ya kuwazia wadau wetu vitalu, TFS ninawapa siku saba mniletee mapendekezo ya kina ni kwa namna gani tunaweza kuwahakikishia wadau wetu ambao ni wawekezaji kwenye viwanda kwa sababu tuna uwezo wa kuwatambua sasa tunawezaje kuweka utaratibu ambao utawahakikishia malighafi kila mwaka walau kwa kipindi kisichopungua miaka mitano ili waweze kukopesheka kwa urahisi ,” amesema.

“Hili ni jambo ambalo halipaswi kushindikana hivyo mjipange mtakavyoweza lakini mtuletee wizarani mapendekezo ni kwa namna gani mtaweka uhakika kwa wadau wetu ambao ni wawekezaji kwenye sekta ya bidhaa ya misitu watapa malighafi kwa uhakika walau katika kipindi cha miaka mitano,” amesema.

Aidha amesema kuwa kwa mwaka Tanzania inaharibu misitu katika eneo la ukubwa wa hekari laki 4.5, ambapo amewapongeza wakazi wa mikoa kusini na baadhi ya mikoa ya Kaskazini na Kaskazini Magharibi kwa jitihada wanazozifanya za kupanda miti kibishara kwa kusema wanasaidia katika ikolojia ya maisha duniani,” amesema Dk. Kigwangalla.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger