Wednesday 31 July 2019

KISANDU ACHAGULIWA KUWA NAIBU MEYA MANISPAA YA SHINYANGA

...



Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga John Kisandu

Na Marco Maduhu - Malunde1 blog Shinyanga

Diwani wa Kata ya Chibe manispaa ya Shinyanga John Kisandu (CCM) amechaguliwa kwa mara nyingine tena kuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, na kumshinda mpinzani wake Zena Gulamu (Chadema).


Uchaguzi huo wa Naibu Meya umefanyika leo Julai 31,2019 kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa baraza la madiwani wa kumchagua Naibu Meya pamoja na Kamati mbalimbali, ambazo zitasimamia utekelezaji wa maendeleo ya Manispaa hiyo, ikiwamo kamati ya fedha ya kudumu, uchumi, elimu na afya, miundombinu, ukimwi, maadili pamoja na Jumuiya ya Serikali za Mitaa (ALAT).

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi, amesema John Kisandu kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ameibuka mshindi kwa kupata kura 15, dhidi ya mpinzani wake Zena Gulam kutoka Chadema ambaye amepata kura tano ,ambapo wajumbe waliopiga kura walikuwa 20.

Akizungumza mara baada ya kupata ushindi huo, Kisandu ameomba ushirikiano kutoka kwa madiwani hao na kuwa kitu kimoja katika kuisimamia halmashauri kwa maslahi mapana ya wananchi na kuwaletea maendeleo.

Aidha madiwani hao wameendelea kujadili ajenda mbalimbali zikiwamo za afya, elimu, maji, miundombinu, fedha, kwa ajili ya mustakabali wa maendeleo ya manispaa hiyo.

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Diwani wa Kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM John Kisandu, akiomba kuchaguliwa kuwa Naibu Meya kwa mara nyingine tena, ambapo alishinda kiti hicho kwa kura 15.

Diwani wa viti wa maalumu Manispaa ya Shinyanga Zena Gulamu kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema(, akiomba kuwa naibu meya wa manispaa ya Shinyanga, ambapo alipata kura tano.

Madiwani wakipiga kura kumchagua Nibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga.

Upigaji kura ukiendelea.

Upigaji kura ukiendelea wa kumchagua Naibu Meya wa manispaa ya Shinyanga.

Upigaji kura ukiendelea wa kumchagua Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga.

Upigaji kura ukiendelea wa kumchagua Naibu Meya wa manispaa ya Shinyanga.

Upigaji kura ukiendelea wa kumchagua Naibu Meya wa manispaa ya Shinyanga.

Naibu meya wa manispaa ya Shinyanga John Kisandu akijipigia kura ya kuchaguliwa kuwa Naibu Meya kwa mara nyingine.

Mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi akimtangaza diwani wa Kata ya Chibe John Kisandu kuwa mshindi wa Kiti cha Unaibu Meya kwa mara nyingine.

Naibu meya wa manispaa ya Shinyanga John Kisandu akizungumza mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho tena, na kuwataka madiwani kushirikiana kwa pamoja kusimamia maendeleo ya halmashauri.

Madiwani wakiendelea na baraza mara baada ya kumaliza kuchaguzi wa Naibu Meya wa manispaa ya Shinyanga na wajumbe wa kamati mbalimbali.

Madiwani wakiendelea na baraza.

Baraza la madiwani likiendelea.

Baraza la madiwani likiendelea.

Diwani wa Kata ya Kitangili Hamisi Ngunila (CHADEMA), akizungumza kwenye baraza hilo.

Diwani wa Kata ya Ndala Wiliamu Shayo(CHADEMA) akizungumza kwenye baraza.

Baraza likiendelea.

Watendaji wa manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye baraza la madiwani.

Watendaji wa manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye baraza la madiwani.

Naibu meya wa manispaa ya Shinyanga John Kisandu, akifunga mkutano wa mwaka wa baraza la madiwani na kuwataka watendaji na madiwani kila mtu awajibike kwenye nafasi yake ili kuleta maendeleo kwenye manispaa hiyo.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger