Saturday 20 July 2019

Taasisi ya elimu ya watu wazima (TEWW) Yajidhatiti Kuwakomboa Vijana Waliokosa Elimu katika Mfumo Rasmi

...
Na Timoth Anderson - TEWW
Taasisi ya elimu ya watu wazima (TEWW) imesema imeweka mkakati wa masomo wa kitaifa ambao utakwenda sambamba na Mpango Changamani kwa Vijana Walio Nje ya mfumo Rasmi wa Elimu maarufu kama ‘IPOSA’ ili kuwafikia  Vijana wa kike na wa kiume ambao hawajawahi kwenda shule, wanafunzi walioacha shule za msingi, wanafunzi waliomaliza darasa la saba lakini hawajapata fursa ya kuendelea, wanafunzi waliohitimu masomo yao kupitia program ya MEMKWA, Wasichana walioacha shule kwa changamoto mbalimbali kama vile ujauzito na ndoa za utotoni

Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Idara ya Elimu kwa Umma Shule Huria, Bw. Placid Balige wakati alikuwa akizungumza na waandishi habari kwenye maonesho ya 14 ya Vyuo vya elimu ya juu sayansi na Teknolojia yanayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja.

"taarifa ya tathmin ya Mpango wa Elimu Changamani baada ya msingi (MECHAM) ya mwaka 2015,Utafiti uliofanywa na Wizara ya Elimu, Sayansi ya Teknolojia wa mwaka 2015 na taarifa ya takwimu ya Elimu ya msingi zinaonesha watoto wa kati ya miaka 14-17 wapatao 2,256,940 hawapo shule japokuwa ilibidi wawepo shule hivyo TEWW, Wizara yetu, wakaanza kuandaa mpango ambao hapana mtoto atakaeachwa kupewa elimu” amesema Balige.

Ameongeza kuwa,  watoto walioingia katika ndoa na mimba za utotoni na kukatisha masomo yao wamepata mafanikio makubwa kwani TEWW kupitia miradi yake mbalimbali wamewafundisha stadi za maisha jambo lililopelekea kuwawezesha kujiajiri wenyewe hali ambayo itawawezesha wale wenye nia ya kurudi shuleni  kwa mfumo rasmi kurudi kwakuwa wameshapewa stadi za maisha juu ya kukabiliana na mazingira yao.

Aidha, Bw. Balige ameongeza kuwa , watoto hao wameweza kufungua maduka na kuweza kudhalisha bidhaa zao wenyewe ikiwemo kutengeneza sabuni, kusindika chakula jambo lililopelekea kupata mkopo wa asilimia 4 wa vijana unaotolewa na Halmashauri katika maeneo yao ili kuwakomboa vijana kiuchumi.

"Tumeweza kuwafikia vijana 3000 katika mkoa wa Dodoma,Rukwa na Lindi ambao walipata ndoa za utotoni na kukatisha masomo yao kwa sasa wameweza hata kujiunga Vikundi na kuweza kupata mkopo wa Manispaa wa asilimia 10 unatolewa nchi nzima " amesema Balige.

Aidha amesema, Taasisi hiyo ilianzishwa na Sheria ya Bunge Namba 12 ya Mwaka 1975 ambapo pamoja na majukumu mengine inatoa Mafunzo kuanzia ngazi ya Astashahada, Stashahada na Shahada katika eneo la Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu pamoja na Ustawi wa jamii kwa njia ya ana kwa ana na kwa njia ya masafa ili kuwaandaa wataalamu wa Elimu ya Watu Wazima hiyo ikiwa ni mtekelezaji wa Ilani ya chama cha Mapinduzi na kwasababu ni mpango mahususi katika kuchagiza Tanzania ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger