Friday 19 July 2019

Rais Magufuli Aiagiza Wizara Ya Katiba Na Sheria Kupitia Magereza Yote Nchini Ili Kuwaachia Wafungwa Wasiostahili Kifungo.

...
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameagiza Wizara ya katiba   na sheria kuendelea kupitia Magereza yote nchini ili kuweza kuwaachia wafungwa wasiostahili kifungo.
 
Rais Magufuli ametoa maelekezo hayo  Julai 18,2019  wilayani Kongwa   mkoani Dodoma wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara.
 
Mhe.Magufuli amesema baadhi ya wafungwa wamekuwa wakifungwa kwa kusingiziwa hivyo ni wakati sasa Umefika Kwa  Wizara kupita  kila gereza na kuchunguza uhalali wa kifungo ili kila mtu apate haki yake kwani serikali ya awamu ya tano ni Wanyonge.

Hivyo ,Rais Magufuli amesema serikali yake hawezi kutawala  kwa kuonea watu  wanyonge huku pia akisisitiza  Umuhimu wa viongozi  wa dini kuliombea taifa la Tanzania .

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amekumbusha Umuhimu wa  kufanya kazi kwa bidii huku akisema asiyefanya kazi na asile na Serikali yake haiwezi kugawa chakula kwa mtu Mzembe.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger