Tuesday 22 January 2019

TETESI ZA SOKA ULAYA JAN 22,2019 , PAUL POGBA KUONGEZA MKATABA MAN U

...

Kiungo wa Manchester United na Ufaransa Paul Pogba , 25, yuko tayari kuketi chini na klabu yake kuzungumzia kuongezwa muda wa mkataba wake. (Sun)

Mshambuliaji wa United na Ufaransa Anthony Martial , 23, yuko karibu kuukubali mkataba mpya ugani Old Trafford. (ESPN)

Arsenal wanachunguza uwezakano wa kumsajili mchezaji wa Real Madrid na Colombia James Ridriguez kwa mkopo. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 kwa hivi sasa yuko kwa mkopo katika klabu ya Bayern Munich. (Independent)

Eden Hazard , 28, amesema hatojiunga na Manchester United hata iwapo Zinedine Zidane atakuchua nafasi ya kuwa meneja na kudokeza kwamba atasalia Chelsea.(Star)

Bayern Munich wanachochewa kutoa ombi la £10m kwa mshambuliaji wa Manchester City na Wales Rabbi Matondo,18, ambaye mkataba wake utakamilika mwishoni mwa msimu.(Sun)Rabbi Matondo( wa pili kutoka kulia) Manchester City

Ombi la West Ham la yuro milioni 40 (£35.28m) lilikataliwa na Atalanta la kumsajili mshambuliaji wa kimataifa Duvan Zapata, 27. (Tuttosport, kupitia Calciomercato)

Cardiff wanajitayarisha kutoa ofa ya £2m kwa mshambuliaji wa Sunderland Josh Maja, lakini paka hao weusi wanahitaji £4m kwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20. (Sun)

Manchester United wangependa kumuajiri mkurugezi wa soka kabla uamuzi maalum kuchukuliwa wa kumuajiri meneja wa kudumu kwa msimu huu. (Independent)

West Ham wamemwambia mshambuliaji Marko Arnautovic, 29, kwamba watamruhusu kuondoka , lakini hawatamuuza mwezi Januari- hata iwapo raia huyo wa Austria akikataa kucheza.(London Evening Standard)

Mshambuliaji wa Chelsea Alvaro Morata anatarajiwa kujiunga na Atletico Madrid kwa mkopo kwa siku zilizosalia za msimu huu , na matarajio ya klabu hiyo ya Ufaransa kumnunua kiungo huyo mwenye umri wa miaka 26.(Sky Sports)

Nahodha wa Paris St-Germain,Thiago Silva amesema haitakuwa makosa kumruhusu kiungo wa kati wa Ufaransa Adrien Rabiot kuondoka katika klabu hiyo. Rabiot, 23, analengwa na klabu tofauti zinazoshiriki ligi ya Premia. (Telefoot, kupitia Talksport)

Mshambuliji wa Fulham Aboubakar Kamara, 23, yuko katika mazungumzo na upande wa Uturuki wa Yeni Malatyaspor kwa mkopo hadi mwishoni mwa msimu huu.(Mail)

Taaluma ya kiungo wa Fulham Kamara inaonekana kufikia kikomo pale kiungo huyo alipoamriwa kufanya mazoezi na klabu ya soka ya wachezaji wenye umri wa chini ya miaka 23. (Telegraph)Aboubakar Kamara wa Fulham

Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy yuko tayari kuchukua £5m kumuuza mshambuliaji Vincent Janssen, 24, mwezi huu, baada ya kumsaini mchezaji wa kimataifa kutoka Uholanzi kwa kitita cha £17m. (Telegraph)

Liverpool wanatarajiwa kuwa klabu ya kwanza ulimwenguni kuripoti faida waliyoipata kwa mwaka ya zaidi ya yuro milioni 100 (£88.3m). (Telegraph)

Winga wa Stewart Downing atajaribu kuutatua mzozo kati yake na klabu ya Middlesbrough wiki hii. Mchezaji huyo wa zamani wa England , 34, ambaye kwa hivi sasa hashiriki katika mchezo wowote kutokana na sababu kwamba klabu hiyo haitaki kujihusisha na mazungumzo ya kumuongezea mkataba wake wa mwaka mmoja, ambao unatarajiwa kuanza baada ya mkataba wa hapo awali. (Mail)

West Brom imehusishwa na beki wa Ipswich Jonas Knudsen, 26, ambaye mkataba wake unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa msimu huu.(Birmingham Mail)

Beki Tosin Adarabioyo, 21, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo na klabu ya West Brom anaweza kurudi Manchester City, kwani klabu hiyo inajaribu kumtafutia nafasi ya kushiriki michezo tofauti katika klabu nyengine.(Birmingham Mail)Romelu Lukaku (kushoto) na Alexis Sanchez (kulia)

Beki wa Stade de Reims Bjorn Engels, 24, ambaye yuko kwa mkopo katika klabu inayoshiriki ligi ya Ligue 1 ya Olympiakos na anahusishwa na Everton , amedokeza itakuwa 'ndoto' kuichezea Arsenal.(Mirror)

Aston Villa inamnyemelea beki wa klabu ya Ufaransa ya Le Havre, Harold Moukoudi, 21, lakini ajenti wa mchezaji huyo amedokeza kwamba mchezaji huyo atajiunga na Ligue 1 msimu huu.(Birmingham Mail)

Mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku , 25, alichapisha kwenye mtandao wa kijamii akikemea fununu za kuihamia Juventus.(Star)

Nottingham Forest wanaonekana kumzingatia kiungo wa kati raia wa Ubeligiji anayeichezea Scunthorpe Funso Ojo, 27 ambaye pia anahusishwa na klabu ya soka ya Derby County.(Nottingham Post)

Millwall wako karibu kufikia makubaliano na maafisa katika eneo la Lewisham kuikubali klabu hiyo kusalia kusini mwa London ili kuimarisha uwanja wao wa nyumbani wa New Den . (Guardian)
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger