
Akizungumza leo Jumatano Januari 16 2019, Lugola pia amemtaka kamanda wa kikosi cha usalama wa barabarani kujitafakari, kujipima kama anatosha katika nafasi hiyo.
"Nimemwelekeza katibu mkuu aunde timu ambayo itapewa miezi mitatu kuchunguza vitendo na mianya ya rushwa na msisitizo mkubwa kwenye usalama wa barabarani na tume hiyo itanipa hatua za kuchukua," amesema.
Amesema kumekuwa na malalamiko mengi yanayohusu ubambikiaji wa makosa ya barabarani kwa madhumuni ya kutaka rushwa na unyanyasaji wa madereva bodaboda.
Ameongeza kwamba licha ya kuwapo makamanda wa trafiki wa mikoa lakini bado kumekuwa na malalamiko juu ya utendaji wa polisi na hivyo ameamua kuchukua hatua dhidi ya vitendo hivyo.
Amesema tume itachunguza kitengo hicho na kumpelekea majibu ili aweze kuchukua hatua.
0 comments:
Post a Comment