Wednesday 2 January 2019

CHELSEA YAMSAJILI MSHAMBULIAJI KINDA WA DORTMUND

...

Klabu ya Chelsea imemsaini mshambuliaji wa Borussia Dortmund Christian Pulisic kwa dau la Yuro 64m lakini itamtoa kwa mkopo kwa klabu hiyo ya Ujerumani hadi mwisho wa msimu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 raia wa Marekani , ambaye alikuwa amehusishwa na vilabu vya Liverpool na Arsenal , alijiunga na Dortumund akiwa mchezaji mchanga 2015.

Pulisic amefunga magoli tisa katika mechi 23 akiichezea Marekani.

''Ilikuwa ndoto ya Christian kujiunga na ligi ya Uingereza'' , alisema mkurugenzi wa klabu ya Dortmund Michaek Zorc.

Hiyo ni kutokana na mizizi yake ya Marekani na kutokana na hilo tulishindwa kuongeza mkataba wake.

''Kutokana na hali hiyo tumekubali ombi zuri la Chelsea''.

Kandarasi ya Pulisic katika klabu ya Dortmund ilitarajiwa kukamilika kufikia 2020.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger