Wednesday 2 April 2014

VIDEO:MAN U YAKAZA MWANZO MWISHO

...



London, England. Manchester United na Barcelona zimeshindwa kutumia vizuri viwanja vyao vya nyumbani baada ya kulazimishwa sare 1-1 na Bayern Munich na Atletico Madrid katika michezo ya kwanza ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa jana.
Manchester United wakiwa kwenye uwanja wao wa Old Trafford, walipata bao la kuongoza dakika 58, kupitia nahodha wake Nemanja Vidic akiunganisha kwa kichwa mpira wa kona, kabla ya Bastian Schweinsteiger kuwasawazishia mabingwa watetezi Munich dakika 67, akimalizia mpira wa kichwa kutoka kwa Mario Mandzukic.
Bayern walipata pigo dakika za mwishoni baada ya kiungo wake Schweinsteiger kupewa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Wayne Rooney.
Kwa mara ya nne mfululizo msimu huu mechi kati ya Barcelona na Atletico Madrid inashindwa kutoa mshindi baada ya jana kutoka sare 1-1 kwenye Uwanja wa Camp Nou.
Neymar aliinusuru Barcelona na kipigo kwa kufunga bao la kusawazisha dakika 71, baada ya Diego kuifungia Atletico goli la kuongoza dakika 56.
Timu zitakazofuzu kwa nusu fainali zitajulikana wiki ijayo kwenye mechi za marudiano.
Leo kuna mechi nyingine mbili za robo fainali kati ya PSG dhidi ya Chelsea na Real Madrid wataonyeshana kazi na Dortmund.
 Jose Mourinho ameitoa Chelsea katika mbio za ubingwa, lakini anaamini vijana wake watathibitisha ubora wao leo dhidi ya Paris Saint-Germain katika mchezo wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger