Tuesday 22 April 2014

Vita ya Mchungaji na Askofu ndani ya Bunge la Katiba

...


Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mchungaji Peter Msigwa.
Ni vita ya maneno ya hoja kati ya Mchungaji Peter Msigwa na Askofu Mstaafu Donald Mtetemela  Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mchungaji Petaer Msigwa amemvaa Askofu Donald Mtetemela na kumtaka avae rasmi magwanda ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza na gazeti hili, Msigwa ambaye pia ni Mbunge kupitia Chadema alisema Askofu Mtetemela alionyesha upendeleo wa wazi kwa CCM alipokuwa akichangia bungeni mjini Dodoma Alhamisi iliyopita.
Katika mchango wake, Askofu Mtetemela alikemea tabia ya wajumbe wa Bunge hilo kuwakashifu waasisi wa Taifa aliosema wana heshima kubwa kwa jamii na mbele za Mungu.
Hata hivyo, Msigwa alisema:“ Askofu ameonyesha upendeleo wa wazi wazi japokuwa anasema anasimamia katikati (hana upande kisiasa). Hakuona kejeli, ubaguzi na matusi yaliyokuwa yakiendelea ndani ya Bunge?”
Mchungaji Msigwa alisema yeye ni mchungaji lakini amejitokeza wazi kusimamia Chadema tofauti na askofu huyo ambaye ameonyesha wazi upande anaousimamia wa CCM, wakati awali walidhani ni mtu mwenye msimamo wa kati.
“Mimi sina ugomvi kama ameamua kuwa mwanasiasa kama mimi lakini awe wazi kwa kusimama na kujionyesha wazi upande aliopo,”alisema.
Kauli ya Askofu Mtetemela
Katika mchango wake, Askofu Mtetemela alilieleza kukerwa na kauli ya Profesa Lipumba kuliita Bunge la Maalum la Katiba kuwa linafanana na kundi ovu la Italahamwe.
“Nasikitika kwamba sijaweza kumuona yeye binafsi Profesa Lipumba ili niweze kumwambia masikitiko yangu, na naamini ni masikitiko ya wengine. Mshtuko wangu ni kwamba alilinganisha Bunge hili na kundi la Intarahamwe la Rwanda,” alisema.
Alibainisha kwamba kihistoria inajulikana Intarahamwe ni wauaji, hivyo sio busara kabisa kuwafananisha wajumbe wa Bunge Maalumu na kundi hilo.
“Hatuko hapa kumuua mtu yeyote, kutuita sisi wauaji si jambo jema, ni baya lakini pia kauli hiyo inaweza kufufua maumivu ya wenzetu wa Rwanda ambao hawataki hali hiyo ijirudie tena katika nchi yao,” alisema.
Alieleza kuwa kauli hiyo pia inaweza kuibua hisia tofauti hata kwa Serikali ya Rwanda inayoweza kufikiri kuwa Tanzania inalifanyia mzaha jambo lililowaumiza kwa kiasi kikubwa.
-mwananchi
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger