Sunday 20 April 2014

LADY JAYDEE ALALAMIKIWA KWA UCHAFU,SOMA HAPA .........

...

MAJIRANI wanaoishi karibu na mwanamuziki wa kizazi kipya Bongo, Judith Wambura ‘Jide’ wamelalamika kwamba mwanamuziki huyo ameiweka nyumba yake katika mazingira ya uchafu yanayohatarisha maisha yao.
Mwanamuziki wa kizazi kipya Bongo, Judith Wambura ‘Jide’.
Wakizungumza na Amani, majirani hao wanaoishi Kimara-Temboni jijini Dar, walisema mwanadada huyo ameacha vichaka vikubwa vinavyoizunguka nyumba yake hali ambayo ni hatari kwani nyoka wanaweza kufanya makazi hivyo kusababisha maafa kwa watoto na watu wazima.
“Yaani huyu mwanamuziki Jaydee ametuachia kichaka, yeye na mumewe hawataki kufanya usafi kuizunguka nyumba yao hali ambayo inatupa wasiwasi sisi majirani, tuna watoto wanaweza kung’atwa na nyoka kwani nyoka hupenda kuzaliana kwenye vichaka kama hivi,”
alisema jirani mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini.
Waliendelea kusema kuwa, Jide hana hausigeli wala ndugu yeyote anayeishi naye, inawezekana ndiyo maana anashindwa kufanya usafi kuzunguka nyumba yake.
“Lady Jaydee anaishi na mumewe (Gardner) tu labda ndiyo sababu ya kushindwa kutunza mazingira, majani yameota mpaka kero. Tumeshapeleka malalamiko yetu serikali ya mtaa lakini hajaitwa kuambiwa, tunashangaa,” alisema jirani huyo.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, gazeti hili lilimtafuta Jide na mumewe Gardner ambapo mume huyo ndiye aliyepatikana na kusomewa madai hayo. Baada ya kusikiliza mpaka mwisho, Gardner alijibu:
“Kama wamesema hivyo mimi sina la kujibu (no comment)”.
Juzi, mapaparazi walifika kwenye ofisi ya serikali ya mtaa lakini ilikuwa imefungwa.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger