Friday 19 July 2019

Marekani Yasema imeidungua ndege isiyo na rubani ya Iran

...
Raisi wa Marekani Donald Trump amesema jeshi la maji la Marekani limetungua ndege isiyo na rubani ya Iran katika eneo la mpaka kati ya ghuba ya uajemi na ghuba ya Oman.

Amesema meli ya jeshi lake ''ilichukua hatua'' siku ya Alhamisi baada ya ndege hiyo kusogea kwa takriban mita 914 karibu na chombo hicho.

Mwezi Juni, Iran iliangusha ndege ya kijeshi isiyo na rubani ya Marekani, na kusababisha hofu ya kutokea mzozo wa kijeshi.

Akizungumza Ikulu, Trump amesema ''Ninataka kuwajulisha kuhusu tukio lililotokea kwenye eneo la mpaka wa Hormuz leo lililohusisha meli yetu ya kijeshi.

"Chombo hicho kilichukua hatua ya kujilinda dhidi ya ndege isiyo na rubani ya Iran ambayo ilikuwa karibu sana hatua iliyokuwa ikitishia usalama wa meli na waliokuwa ndani ya meli hiyo. Ndege hiyo iliharibiwa mara moja''.

"Hili ni tukio miongoni mwa matendo mengine ya uchokozi unaofanywa na Iran dhidi ya meli zinazokuwa kwenye maji ya kimataifa. Marekani in haki ya kujitetea, na kutetea maslahi yake''.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger