Friday 19 July 2019

Iran Yakana Marekani Kuitungua Ndege Yake Isiyo Na Rubani

...
Iran imekanusha madai ya Rais Donald Trump wa Marekani kwamba meli ya kivita ya nchi yake imeharibu ndege isiyo na rubani ya Iran karibu na Ghuba ya Uajemi baada ya kuitishia meli hiyo, tukio ambalo linaonesha ongezeko jipya la wasi wasi kati ya nchi hizo chini ya mwezi mmoja baada ya Iran kuitungua ndege kama hiyo ya Marekani katika eneo na kumfanya Trump kukaribia kulipiza kisasi kwa mashambulizi ya kijeshi. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameandika katika ukurasa wa Twitter kuwa Iran haijapoteza ndege yoyote isiyo na rubani katika ujia wa maji wa Hormuz ama kwingine kokote. 

Waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Mohammad Javad Zarif amesisitiza hakuna ndege isiyo na rubani iliyopotea hadi sasa.

Trump jana alisema meli ya USS Boxer ilichukua hatua za kujihami baada ya ndege isiyo na rubani ya Iran kukaribia karibu yadi 1,000 kutoka meli hiyo na kupuuzia miito kadhaa ya kuondoka.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger