Saturday 2 February 2019

MWALIMU MKUU ATUPWA JELA KWA WIZI WA FEDHA ZA SHULE

...
Mwalimu Mkuu shule ya sekondari Mikwambe, Paulo Lorry, amehukumiwa kifungo cha miaka sita na kutakiwa kulipa Sh milioni 16 katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke alizoiba kutoka akaunti ya shule.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Taasisiya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Temeke, Pilly Mwakasege, ilieleza kuwa mwamu Lorry amekutwa na hatia na kuhukukiwa kwenda jela.

Ilieleza kuwa mwalimu huyo alishtakiwa na makosa matatu ya matumizi mabaya ya ofisi kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11/2007 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Mshitakiwa alikuwa ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mikwambe Manispaa ya Temeke mwaka 2010 alipokea Sh milioni 28 kupitia akaunti ya shule namba CA 2011100236 kwa ajili ya ujenzi wa maabara shuleni hapo.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger