Tuesday 26 February 2019

MBUNGE WA CCM AFUNGUKA BAADA YA NDOA YAKE KUVUNJIKA

...

Mbunge Bonnah Kaluwa

Mbunge wa Segerea (CCM) jijini Dar es Salaam aliyekuwa akitumia jina la Bonnah Kaluwa amekiri kuachana na mume wake Moses Kaluwa na hivyo kulazimika kubadili majina yake ya mwisho.

Mbunge huyo wa CCM ambaye katika mitandao yake ilikuwa ikifahamika kwa jina la Bonnah Kaluwa sasa yanasomeka kama 'Bonnah Kamoli'.

Hata hivyo baada ya tetesi hizo kusambaa kwa kasi, kupitia gazeti linalotoka kila siku Bonna amekiri ukweli wa taarifa hizo.

“Taarifa ni za kweli tumeachana. Ni matatizo ya kifamilia. Nimeshaweka majina yangu kwenye mitandao ya kijamii. Nimeweka Instagram, Facebook. Bunge wana taratibu zao, si wamepata barua", amesema Bona.

Hata hivyo tovuti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bado imeendelea kutumia majina yake ya awali ya ‘Bonnah Moses Kaluwa'.
Chanzo - EATV
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger