Tuesday 26 February 2019

MTU NA DADA YAKE WAFARIKI KWA KUPIGWA SHOTI YA UMEME WAKIANIKA NGUO

...

Watu wawili wa familia moja, Zulfa Chami na Zuhura Chami wamepoteza maisha, baada ya kupigwa shoti ya umeme na kamba ya kuanikia nguo katika eneo la Pasua, Manispaa ya Moshi.

Zulfa (24) na Zuhura (28) wamefikwa mauti hayo leo wakati wakianika nguo.

Habari zilizopatikana kutoka eneo la tukio na baadae kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi, Hamisi Issah zinaeleza kuwa ndugu hao wa familia moja walifariki dunia papo hapo baada ya kupigwa shoti ya umeme.

"Ni kweli ni mtu na dada yake wamefariki dunia leo kati ya saa 3:00 na 3:30 asubuhi katika eneo la Pasua Manispaa ya Moshi", amesema Kamanda Issah.

Chanzo - Nipashe
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger