Monday 25 February 2019

WATUMISHI WA SERIKALI WALIOFARIKI KWA AJALI YA GARI MTONI WAAGWA

...



Miili ya wataalam tisa wa idara ya ardhi na idara nyingine za Serikali waliofariki kwa ajali ya gari baada ya kutumbukia Mto Kikwawila , inaagwa leo Februari 25, katika viwanja vya Can, Tangani mjini Ifakara.

Kwenye tukio hilo Viongozi mbali mbali wa serikali wamehudhuria, akiwemo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula, mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kebwe, pamoja na wafanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero na Ifakara.

Ajali hiyo ilitokea Jumamosi ya Februari 23 saa 11 jioni katika Mto Kikwawila baada ya gari aina ya Toyota Land Cruiser Hard Top linalomilikiwa na wilaya ya Kilombero, kutumbukia kwenye mto huo na kusababisha vifo vya watumishi hao wa kitengo cha upimaji ardhi, huku wanne wakijeruhiwa.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger