Sunday 24 February 2019

RAIS WA KOREA KASKAZINI ATUMIA TRENI KWENDA VIETNAM KUKUTANA NA RAIS TRUMP

...
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un yumo ndani ya treni akielekea nchini Vietnam kwa ajili ya mkutano wake wa pili wa kilele na rais Donald Trump wa Marekani. 

Kim ameambatana na Kim Yong Chol, ambaye ndie mpatanishi muhimu katika mazungumzo na Marekani. Mkutano wa pili baina ya Kim na Trump umepangwa kufanyika Jumatano na Alhamis wiki ijayo mjini Hanoi. 

Mkutano wa kwanza uliofanyika nchini Singapore mwezi Juni, ulimalizika bila ya makubaliano muhimu juu ya kusistishwa miradi ya kinyukilia ya Korea Kaskazini. 

Katika mkutano huo, wataalamu wanasema Kim atajaribu kuimarisha mahusiano na Marekani pamoja pia na kuondolewa vikwazo. Safari za nje za kiongozi huyo wa Korea Kaskazini kawaida hupangwa kwa siri. 

Zaidi ya siku mbili zitahitajika kwa treni anayosafria Kim kuzunguka masafa ya maelfu ya kilomita kupitia mji wa mpakani wa China-Dandong hadi Vietnam.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger