Wednesday 27 February 2019

CHAMA CHA WAIGIZAJI KINONDONI ( KAMAMIKI ) CHAMLILIA RUGE

...
Chama cha Waigizaji Kinondoni, kimetoa pole zake kwa kifo cha  Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group, Ruge Mutahaba aliyefariki jana Jumanne Februari 26,2019.

Katika taarifa yao iliyosainiwa na  Mkuu wa Idara ya Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, Masoud Kaftany imesema enzi ya uhai wake, Ruge alitoa mchango mkubwa kwa  wasanii wa muziki na fani zingine na kutoa elimu ya ujasiriamali

Pia alitoa mchango kwa Taifa la Tanzania katika nyanja ya muziki ambazo zilikuwa  chachu kubwa ya kujenga na kuandaa jamii ya Kitanzania kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaendeleo, kiuchumi, kisiasa na kijamii katika ujenzi wa taifa.

==>>Hii ni taarifa yao 
*Kamati ya Matukio Maadili na mikataba ya Chama cha Waigizaji ( M) Kinondoni ( KAMAMIKI ) Inatoa pole kwa *CLOUDS MEDIA GROUP na Familia Ya Marehemu *RUGE MUTAHABA* Kwa kuondokewa na Mpendwa Wetu Ruge Mutahaba ambaye Enzi za Uhai wake alikuwa Mwasisi na Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media

Enzi ya uhai wake *Ruge* alitoa mchango Mkubwa Kwa Wasanii wa Muziki na Fani zingine na kutoa Elimu ya Ujasirimali kwa Taifa La Tanzania Katika Nyanja Ya Muziki , ambazo Zilikuwa Chachu Kubwa ya Kujenga na Kuandaa Jamii ya Kitanzania Kukabiliana na Changamoto Mbali Mbali za Kimaendeleo , Kiuchumi , Kisiasa na Kijamii Katika Ujenzi wa Taifa.

Tunamuombea Kwa Mungu apumzike kwa Amani kwenye Nyumba Yake ya Milele. 

Bwana Ametoa , Bwana Ametwaa , Jina la Bwana Lihimidiwe . Inna Lillah wa Inna Illayhi Raj'uun. Asante. 

Imetolewa Na; Mkuu wa Idara ya Habari , Uenezi na Mahusiano na Umma - TDFAA ( KINONDONI ). *Masoud kaftany*
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger