Tuesday 26 February 2019

SHIRECU YAENDELEA KUFANYA UKARABATI MKUBWA WA MAGARI YAKE KUJIANDAA NA MSIMU MPYA WA PAMBA

...

TAARIFA KWA UMMA
Katika kuelekea msimu mpya wa pamba wa mwaka 2019/2020 Chama Kikuu cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Region Co-Operative Union (1984) Ltd - SHIRECU) kimeweza kufanya marekebisho magari yake ili kujiandaa na msimu wa pamba wa mwaka 2019/2020.

Ukarabati huo unajumuisha magari makubwa na madogo,ambapo kati ya magari makubwa 30 yenye uwezo wa kubeba tani 10 hadi 15,magari makubwa matatu yamekarabatiwa na mengine yanaendelea na ukarabati,aidha magari madogo matatu(3) kati ya 13 aina ya land cruiser hardtop 1 hz yamekarabatiwa na kuendelea kufanya shughuli za kila siku za union.

Ukarabati huo umelenga kuandaa magari kwa ajili ya kuwasaidia wakulima kupitia vyama vya msingi kupata huduma ya uchukuzi katika msimu wa pamba unaotarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.

Aidha pia magari hayo makubwa yatatumika kwa kukodishwa na watu binafsi ili kuweza kuongeza mapato kwa chama kikuu cha ushirika mkoa wa Shinyanga.

Imetolewa na: 

Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano 
Shinyanga Regional Cooperative Union (SHIRECU(1984)LTD). 
26.02.2019.
Magari yaliyokarabatiwa na SHIRECU
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger