Saturday 2 February 2019

BABA MZAZI AWAPACHIKA MIMBA MABINTI ZAKE WAWILI

...
 Baba wa mabinti wawili mjini Eldoret nchini Kenya anasakwa na maafisa wa polisi baada ya kuwabaka na kuwapachika mimba watoto hao kwa wakati tofauti.

Baba huyo anasemekana kuanza kuwabaka wanawe mwaka wa 2014 mama yao alipoaga dunia.

 Mshukiwa alikuwa amerejea nyumbani kutoka gerezani baada ya kukamatwa kwa kumbaka binti wake kitinda mimba.

 Kulingana na taarifa za Citizen TV, jamaa huyo alipofika nyumbani kwake, alimbaka tena bintiye mkubwa ambaye kwa sasa amempachika pia mimba. 

 Msichana huyo aliwambia wanahabari kuwa dadake mdogo alijitoa uhai mwaka wa 2018 akiwa na ujauzito wa miezi saba. 
Msichana huyo ambaye pia ni mjamzito, alisema aliwasilisha malalamishi yake kwa wazee wa kijiji ila hakuna hatua ambayo imechukuliwa dhidi ya baba yao

 Aliamua kuranda katika mitaa ya mji wa Eldoret ila wasamaria wema wajitokeza na kumpa makazi.

Wasichana hao wamekuwa wakiteseka mikononi mwa baba yao ambaye anapaswa kuwalinda tangu mama yao alipofariki mwaka wa 2014.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger