Friday 26 June 2015

Kafulila awalipua mawaziri ufisadi mabehewa,ingia hapa kujua alichosema

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Awali mapema asubuhi aliomba mwongozo ripoti ya uchunguzi kuhusu ufisadi wa bilioni 238 za ununuzi mabehewa feki iletwe lakini spika kapangua akasema kamati ndio ina haki ya kuleta bungeni na sio mbunge.
Kwa mujibu wa Kafulila wakati akichangia mara ya pili alisema ufisadi huu unahusu Wizara ya Uchukuzi na Wizara ya Fedha. Hivyo Mwakyembe, katibu mkuu, Waziri Fedha na Katibu Mkuu wa Wizra ya Fedha wote wanahusika kwani mlipaji mkuu ni Wizara ya Fedha sasa inawezekanaje malipo yafanyike kabla ya mabehewa kuletwa kama sio ufisadi. 
Alihoji zaidi kwanini Spika hataki serikali ilete ripoti hiyo bungeni ili mbivu na mbichi zijulikane au kwa sababu ni kipindi cha lala salama imebaki kila waziri anakwapua tu wizarani kwake?.
"Nasisitiza ripoti ya wizi huu ni lazima iletwe bungeni ili bunge lijadili na kuamua. Hamuwezi kudanganya watu kwamba mnaongeza kodi kwenye mafuta ili mpate pesa za miradi ya umeme wakati kuna zaidi ya bilioni 238 zinapotea", alisema.
Ripoti ya PPRA ipo wazi kwamba kampuni ya India ya Hindustan ilipewa zabuni bila kufanya uchunguzi wa uwezo na weledi wa kampuni hii, kwamba Wizara ya Fedha ilifanya malipo yote kabla ya mabehewa kuletwa. Na mbaya zaidi mabehewa yaloletwa ni feki. Sasa kwanini serikali iendelee kuficha?.
Kwanini bunge nalo linajinyima meno kuchukulia hatua watu hawa?
Pia alimtaka Spika wa Bunge kuwa sehemu ya bunge na sio serikali.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger