Thursday, 7 February 2019

NDUGAI ASEMA KUNA HAJA YA KUSIMAMISHA MSHAHARA WA TUNDU LISSU

...
Spika wa Bunge, Job Ndugai (Mb) amesema kuna haja ya kusimamisha mshahara wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa sababu hayupo bungeni, jimboni kwake wala hospitalini, na hajapewa taarifa zozote na daktari.

Spika Ndugai ametoa taarifa hiyo Bungeni wakati akijibu Muongozo wa Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Msukuma ambapo amesema Mbunge huyo hayupo Hosipitali,Hayupo Bungeni na hayupo Tanzania wala hajulikani anafanya kitu gani huko aliko hivyo hana sababu ya kuendelea kulipwa.

Tundu Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, yupo katika ziara ya siku 10 nchini Marekani baada ya kufanya hivyo kwenye nchi za Ujerumani na Uingereza.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger