Monday, 4 February 2019

AMUUA MKEWE KWA KUMNYONGA AKIMTUHUMU KUCHEPUKA NA WANAUME WANAOMPA POMBE KAHAMA

...

Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Maselle Mheziwa (40) mkazi wa Kagongwa wilayani Kahama ameuawa kwa kunyongwa shingo na mmewe aitwaye Omary Juma (46),mkazi wa Kagongwa kutokana na ugomvi wa wivu wa kimapenzi.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao,tukio hilo limetokea Februari 2,2019 majira ya saa mbili asubuhi katika kata Kagongwa, tarafa ya Isaghehe, wilaya ya Kahama.

 "Chanzo ni ugomvi uliokuwepo kati ya marehemu na mumewe akimtuhumu mkewe kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wengine kwa sababu ananunuliwa pombe na wanaume bila kibali kutoka kwa mmewe",amesema Kamanda Abwao.

"Mbinu iliyotumika ni kumnyonga shingo na kumweka njiani ili asijulikane. Mtuhumiwa amekamatwa kwa hatua zaidi za kisheria",ameongeza.

Na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.


Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog


Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install


https://bit.ly/2Qb7qyF



NB: App uliyokuwa unatumia mwanzo tumeifuta na kuleta mpya ya kisasa zaidi..Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger