Na Mwandishi wetu, Ngara. Naibu waziri wa maji,Juma Aweso ameahidi wizara yake kuwalipa wakandarasi wa miradi ya maji inayofadhiliwa na benki ya dunia katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera kiasi cha Sh433.46 milioni baada ya kucheleweshewa fedha hizo kutoka serikalini tangu mwaka 2014. Naibu waziri huyo pia amepongeza uongozi wa wilaya hiyo kwa kusimamia miradi ya maji katika vijiji inayofadhiliwa na benki ya dunia na kwamba halmashauri hiyo imedhibiti matumizi mabaya ya fedha za serikali zinazoelekezwa kwa wananchi kupata maji safi na salama. Aweso ametoa pongezi hizo Januari 13, 2019…
0 comments:
Post a Comment