Saturday 29 December 2018

Ben Paul, Depay, uso kwa uso Dubai

...

Kupitia ukurasa wa star wa Bongo Fleva @iambenpol nimeona picha akiwa na star wa zamani wa Manchester United @memphisdepay kwa sasa anacheza Lyon ya Ufaransa.

Nikatamani kujua Ben Paul amekutanaje na Depay na kama walipiga story hadi kufikia kupiga picha. Ndugu yetu akanisimulia mwanzo mwisho mambo yalivyokuwa.

“Nimekutana nae hapa Dubai kwenye hotel ambayo nimefikia, nimeingia hapa juzi yeye sijui yupo hapa tangu lini.”

Jana wakati naenda kupata lunch ndio nikakutana nae, yeye pia alikuwa anaenda lunch…akaniangalia halafu akasema: “Wewe kuna rafikiyangu umefanananae.”

“Nilikuwa sijamjua nikawa najiuliza huyu jamaa ni nani lakini sura yake ilikuwa inaniijia baada ya kumkaribia nikamuuliza wewe ni Memphis akasema ndiyo yeye na pale yupo holiday.

“Tukaongea kidogo masuala ya muziki akasema ametoa wimbo, nikaangalia instagram yake nikaona, baada ya hapo tukapiga story kidogo na picha tukaenda kula chakula tukaachana.”

“Story nyingi zilikuwa kuhusu muziki, anauliza Afrika vipi tunafanyaje, tukabadilishana mawasiliano tutakuwa tunawasiliana labda baadaye chochote kinaweza kutokea.”



from ShaffihDauda http://bit.ly/2EVDOnx
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger